Wachezaji watano watakaoshindania Tuzo ya BBC ya Mwanakandanda Bora wa Afrika wa Mwaka 2016 wametangazwa.
Wachezaji hao ni Pierre-Emerick Aubameyang, Andre Ayew, Riyad Mahrez, Sadio Mane and Yaya Toure.
Wachezaji hao watano walitangazwa wakati wa kipindi maalum cha moja kwa moja runingani Jumamosi.
Piga kura hapa : bbc.com/africanfootball
Mshindi
atachaguliwa na mashabiki wa soka ya Afrika kutoka kila kona ya dunia.
Mashabiki wana hadi saa 18:00 GMT tarehe 28 Novemba kumpigia kura
mchezaji wanayempenda.
Mnamo Jumatatu, 12 Desemba, mshindi wa tuzo
hiyo atatangazwa moja kwa moja kwenye runinga ya BBC Focus on Africa
pamoja na redio, kuanzia saa 17:35.
Tovuti za BBC Swahili, BBC Sport na BBC Africa pia zitachapisha habari za mshindi.
Aubameyang
ameorodheshwa kwa mwaka wan ne mtawalia, mshindi wa mwaka 2011 pia
ameorodheshwa kwa mwaka wa nne, Mahrez ndiye mchezaji pekee ambaye
hajawahi kuorodheshwa kushindania, Mane alishindania mara ya kwanza
mwaka jana naye mshindi mara mbili. Toure ameorodheshwa kwa mwaka wa
nane mtawalia.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon Aubameyang
amekuwa na kipindi cha kufana sana mwaka 2016, amefunga mabao 26
(kufikia wakati wa kuandika makala hii) katika klabu yake ya Borussia
Dortmund nchini Ujerumani
Alikuwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika
kutawazwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka wa Bundesliga, raia wa kwanza wa
Gabon kushinda Tuzo ya Shirikisho la Soka Afrika ya mchezaji bora wa
mwaka Afrika, na ameorodheshwa miongoni mwa wachezaji wanaoshindania
tuzo ya mchezaji bora duniani mwaka 2016, tuzo ya Ballon d'Or.
Mwezi Agosti West Ham walivunja rekodi yao ya
kununua wachezaji, walipolipa Swansea £20.5m kumchukua nyota wa Ghana
Ayew, ishara tosha ya kiwango kizuri cha kiungo huyo wa kati mwaka mmoja
uliopita.
Ayew amekuwa akicheza vyema sana, na magoli 12
aliyoyafunga msimu wa 2015/16 mechi 35 alizochezea Swansea, ulimfanya
kuitwa mchezaji bora mgeni wa klabu hiyo wakati wa tuzo za mwisho wa
msimu mwezi Mei.
Mchezaji mwingine wa Ligi Kuu ya England anayechezea
Leicester City, Mahrez kutoka Algeria alifana sana na kutekeleza
mchango mkubwa kwa klabu yake - ambayo uwezekano wake wa kushinda mwanzo
wa msimu ulikuwa 5,000-1- na kuiwezesha kushinda ligi mara ya kwanza.
Mahrez
alifunga mabao 17 ligini msimu wa 2015/16 na alichaguliwa na Chama cha
Wachezaji wa Kulipwa Uingereza kuwa Mchezaji Bora wa mwaka - Mwafrika wa
kwanza kushinda tuzo hiyo.
Kadhalika, aling'aa na kusaidia Algeria kufuzu kwa Kombe la Taifa Bingwa Afrika 2017.
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka Senegal Mane
aliibuka mchezaji ghali zaidi katika historia ya soka Afrika aliojiunga
na Liverpool kwa £34m majira ya joto mwaka huu.
Uchezaji wake
ulidhihirika mara moja uwanjani Anfield, ambapo aliwafungia Liverpool
mabao sita na kusaidia ufungaji wa mengine manne katika mechi 11. Ni
kama aliendeleza kutoka alipoachia Southampton, ambapo alikuwa amefunga
mabao manane ligini akichezea Saints mwaka 2016, ikiwa ni pamoja na
mabao matatu aliyoyafunga dhidi ya mabingwa wa wakati huo Manchester
City,
Toure alijishindia kombe jingine mwaka 2016, kombe
lake la 17 katika maisha yake ya uchezaji, aliposhinda Kombe la Ligi
Uingereza akiwa na Manchester City, ambapo alifunga penalti ya ushindi
wakati wa matuta dhidi ya Liverpool kwenye fainali.
Huu ulikuwa
mwaka ambao kigogo huyu wa safu ya kati kutoka Ivory Coast, ambaye sasa
ana miaka 33, alistaafu soka ya kimataifa baada ya ufanisi mkubwa lakini
bado akajidhihirisha kwamba hajaishiwa na nguvu ya kucheza na
kujumuishwa kwenye orodha hii kwa mwaka mwingine kunatilia mkazo hili.
0 comments:
Post a Comment