Yanga wamefanikiwa kumaliza vyema mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kwa kuwatandika Maafande wa Ruvu Shooting mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Saimon Msuva na Haruna Niyonzima, wakati la Ruvu Shooting lilipachikwa kambani na Abdulrahman Mussa.
Hii ilikuwa mechi ya mwisho kwa kocha wa Yanga, Mholanzi, Hans van der Pluijm ambaye anampisha Mzambia, George Lwandamina anayetarajiwa kuanza kazi mzunguko wa pili.
0 comments:
Post a Comment