Tuesday, November 8, 2016

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai kutokana na kifo cha Spika Mstaafu wa bunge hilo la Tanzania, Samwel Sitta.

 Mzee Sitta ambaye ni Mbunge wa zamani wa Jimbo la Urambo lililopo mkoani Tabora amefariki dunia usiku wa kuamkia Novemba 7, 2016 kwenye Hospitali ya Chuo Kikuu cha Technical iliyopo Munich nchini Ujerumani usiku wa kuamkia Novemba 7, 2016.

Rais Malinzi amesema kwamba Sitta ameacha alama ya ucheshi na upenzi katika michezo hususani soka kwani enzi zake hakuficha mapenzi yake kwa klabu ya Simba alikokuwa mwanachama.

Salamu za rambirambi za Rais Malinzi zimekwenda pia kwa Rais wa Klabu ya Simba, Evance Aveva, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki. Amewataka kuwa watulivu wakati huu mgumu wa kumpoteza Mzee Samwel Sitta na kwamba anaungana nao kwenye maombolezo.

Akimwelezea zaidi Mzee Sitta, Rais Malinzi amesema kwamba "Binafsi nitamkumbuka na kuenzi uchapakazi wake. Alikuwa Mwanamichezo aliyekuwa na Mzalendo hususani alipokuwa Spika wa Bunge kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2010 na alikuwa pia Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Aliwahi kuwa waziri katika wizara mbalimbali kwa vipindi tofauti.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina la Bwana Lihimidiwe.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video