Sunday, November 6, 2016


Na Samuel Samuel
Safu ya ulinzi ya African Lyon  leo itakuwa na kibarua cha aina yake kuizuia safu ya ushambuliaji ya Simba SC yenye uchu mkubwa wa kuipatia ubingwa timu hiyo msimu huu bila kupoteza mchezo hata mmoja.
Shiza Kichuya kiungo mshambuliaji wa pembeni wa Simba SC anaongoza katika orodha ya wafungaji wa ligi kuu kwa mzunguko huu wa kwanza wa ligi, akiwa na goli 9 kibindoni. Huyu ndie anatazamiwa kuwa mwiba mkali kwa wageni wa ligi African Lyon akiwa na uwezo wa kufunga, kuchezesha wenzake pia kusaidia kukaba.
Ukiangalia orodha ya wafungaji bora 10 wa ligi kuu , Kichuya ndio mchezaji pekee anaeingia katika orodha hiyo kutokea Simba SC tofauti na mpinzani wao African Lyon ambaye hana hata mchezaji mmoja.
Kocha wa African Lyon mreno Bernardo Tavares anaetumia mfumo wa 4-4-2 anaposhambulia na 4-5-1 timu inapojilinda, ana kazi ya ziada kukiongoza kikosi chake kuibuka na ushindi dhidi ya Simba SC chini ya Joseph Omog ambaye ameweza kukiongoza kikosi chake katika michezo 13 kushinda michezo 11 na kutoka sare michezo 2.
Hood Mayanja ndio mchezaji tegemeo katika kikosi cha African Lyon akiwa na goli 3 mpaka sasa ambaye mwalimu Bernardo mara kadhaa amekuwa akisuka kikosi chake kumzunguka yeye mwenye uwezo mzuri kuisumbua ngome ya wapinzani kwa mashuti yake na kuicheza mipira iliyokufa ingawa ubovu wa safu ya kiungo ya African Lyon na eneo la ulinzi , umeifanya timu hiyo kupoteza michezo mingi na kujikuta wakiangukia nafasi ya 11 katika ligi baada ya kucheza michezo 14 wakishinda michezo 3 tu , sare 5 na kufungwa michezo 6.
African Lyon wana uwezo wa kuizuia Simba SC wakijipanga vyema eneo la kiungo na safu yao ya ulinzi. Kocha mkuu wa Simba SC ana utofauti mkubwa na waalimu wengi ndani ya ligi kuu ambao wanazitengeneza timu zao kuwazunguka " key players" kusaka ushindi.
Omog ameisuka Simba SC katika mfumo ambao mchezaji yoyote aliyeko katika safu ya ushambuliaji ana uwezo wa kufunga .
Jonasi Mkude kiungo wa chini wa Simba SC ndio roho ya timu hiyo katika kujilinda na kushambulia. Yeye ndie anaamua goli lipatikane kupitia upande upi na anasimama imara kuwalinda walinzi wake wa kati.
Lyon wanahitajika kuipasua Simba SC kuanzia eneo la kiungo alipo Mkude , Mzamiru na kiungo mchezeshaji Mwinyi Kazimoto. Wakiweza kuikataa Simba kujenga mashambulizi yake tokea kati basi wanaweza kuifunga timu hiyo au kutoa sare.
Unapocheza na timu kubwa inayokuzidi sana kimbinu na kiufundi lazima ujipange vyema kwenye hesabu zako hususani katika ulinzi na kushambulia.
Mbeya City walifanikiwa kuilaza Yanga SC kwa goli 2-1 kwa kuchukua tahadhari mapema ambayo pia Lyon wakiitumia wanaweza kuwazuia Simba SC .
Cha kwanza ni kujiandaa vyema kisaikolojia katika kupambana muda wote kusaka ushindi na kukataa hali ya unyonge. Hili huleta makini katika kusimamia mfumo husika wa mwalimu katika kujilinda na kushambulia.
Pili ni kupata mbinu rafiki za kuwatoa mchezoni wapinzani wenu na kuhakikisha wanaingia katika mtego wa paniki ili kuua uelewano wa kimbinu uwanjani.
Mwisho matumizi sahihi ya kila nafasi mnayoipata langoni mwa mpinzani wenu hususani mashambulizi ya kushitukiza na mipira iliyokufa.
Simba SC ni wazuri sana kwa kushambulia wakijenga pasi fupi fupi za kasi tokea kati lakini kwa timu makini katika kushambulia hususani kwa mipira mirefu ya krosi tokea pembeni , unaweza ifunga timu hii kutokana na uwezo mdogo wa kipa wao Vicent Agban kucheza krosi na kufanya timing katika kutoka kwenye one against one . Uchache wa magoli 3 mpaka sasa aliyofungwa , unabebwa vyema na uimara wa beki yake.
Tukiangalia upande wa Simba SC yenye uchu mkubwa kutwaa ubingwa msimu huu wa 2016-17 ni ngumu kidogo kupoteza mchezo huo ukilinganisha uwezo wao kimbinu na kiufundi dhidi ya African Lyon.
Wameshinda mechi 11 na wakitoka sare mara mbili tu ! hii peke yake inawajenga vyema kisaikolojia kuusaka ushindi wa 12 katika mchezo wa kesho.
Mfumo wa ushambuliaji wa timu hiyo unaojengwa na viungo makini kama Jonasi Mkude , Mzamiru , Mwinyi Kazimoto na kiungo mshambuliaji anaekuja kwa kasi hivi sasa Mohamedi Ibrahimu anaesimama kama Play maker na mshambuliaji namba mbili , unaifanya safu ya ushambuliaji ya Simba SC kuwa tishio .
Lyon wana matatizo katika kujipanga katika safu yao ya ulinzi hii imewafanya kupoteza mechi 6 na magoli mengi ya kufungwa, Simba ni wazuri kutumia nafasi na kuwavuruga wapinzani kwa mashambulizi yao ya kasi , hii inanifanya nione kesho Lyon kama hawatakuwa makini watawapa fursa Simba kucheka na nyavu.
Bukungu upande wa kulia na Zimbwe Jr kushoto ni hazina kubwa ya Simba SC katika mfumo wao wa 4-4-2 ambao unaruhusu walinzi wa pembeni kupanda juu kusaidia mashambulizi . Lyon wana kazi ya ziada kuzuia mshambulizi ya upande yenye kasi toka kwa wachezaji hawa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video