Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali na wa kusisimua, kila timu ilianza kucheza kwa tahadhari kubwa ili kutoruhusu bao la mapema na kujiweka katika mazingira magumu.
Dakika ya 32, Mbuyu Twite alilimwa kadi ya njano baada ya kumfanyia faulo Benjamin Asukile na mwamuzi kumpa adhabu hiyo.
Dakika ya 45 kinda wa Yanga Yusufu Mhilu alikosa bao baada ya shuti lake kupaa nje ya lango la Prisons.
Kipindi cha kwanza kiliisha huku kila upande ukitoka bila kuona lango la mpinzani wake.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kutokana na Prisons kuamua kushambulia hali iliyopelekea mchezo kuwa mgumu kwa pande zote mbili.
Kutokana na hali kuzidi kuwa ngumu Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Yusufu Mhilu na nafasi yake kuchukuliwa na Simon Msuva.
Prisons walipata penati baada ya Deus Kaseke kufanya madhambi katika eneo la hatari, lakini penati iliyopigwa na Lambert Sabianka iliokolewa na Beno Kakolanya.
Dakika ya 60 Amissi Tambwe aliingia kuchukua nafasi ya Deus Kaseke.
Yanga walipata penati kufuatia mshambuliaji wao Mzambia Obrey Chirwa kuangushwa kwenye eneo la penati na Simon Msuva kuukwamisha mpira wavuni na kuipa Yanga bao la ushindi.
Mwamuzi alikataa kutoa penati kwa Yanga baada ya Donald Ngoma kufanyiwa faulo ya wazi na beki wa Prison dakika za majeruhi.
Mpaka filimbi ya mwisho inapulizwa, Yanga waliibuka kifua mbele kwa ushindi wa bao 1-0. Matokeo hayo yanaifanya Yanga kuendelea kuwa mbabe wa Prisons baada ya kuibuka na ushindi katika michezo mingi waliyokutana hivi karibuni.
Matokeo mengine
African Lyon 1-0 Simba SC
Mfungaji: Abdallah Msuhi
Mbao FC 2-1 Azam FC
Wafungaji:
Mbao: Venance Ludovick na Boniface Maganga
Azam: Fransisco Zekumbawira
Ndanda FC 2-1 Stand United
Wafungaji:
Ndanda: Riphat Khamis (Penati) na Ahmed Msumi
Stand: Frank Khamis
Kagera Sugar 3-1 Ruvu Shooting
Wafungaji:
Kagera Sugar: Them Felix, Seleman Mangoma na Mbaraka Yusuf
Ruvu Shooting: Said Dilunga
JKT Ruvu 1-1 Toto African
Wafungaji:
JKT Ruvu: Saad Kipanga
Toto African: Waziri Junior
Matokeo mengine
African Lyon 1-0 Simba SC
Mfungaji: Abdallah Msuhi
Mbao FC 2-1 Azam FC
Wafungaji:
Mbao: Venance Ludovick na Boniface Maganga
Azam: Fransisco Zekumbawira
Ndanda FC 2-1 Stand United
Wafungaji:
Ndanda: Riphat Khamis (Penati) na Ahmed Msumi
Stand: Frank Khamis
Kagera Sugar 3-1 Ruvu Shooting
Wafungaji:
Kagera Sugar: Them Felix, Seleman Mangoma na Mbaraka Yusuf
Ruvu Shooting: Said Dilunga
JKT Ruvu 1-1 Toto African
Wafungaji:
JKT Ruvu: Saad Kipanga
Toto African: Waziri Junior
0 comments:
Post a Comment