Kocha mkuu
wa Yanga, Hans van der Pluijm ambaye
anadaiwa kuwa wachezaji wake katika mechi ya jana waliyoshinda mabao mawili kwa
moja dhidi ya Ruvu Shooting, amesema bado ni mapema kusema amejiuzulu kwa mara
nyingine kwasababu anasubiri kikao na mwenyekiti wa klabu, Yusuf Manji.
“Kwanza
ni kuingilia kwa rafiki yangu waziri wa
mambo ya ndani…tulifanya vikao…tukawa na kikao pia na Mwenyekiti. Alinishawishi
kuendelea. Pia nadhani jambo la muhimu zaidi ilikuwa ni muitikio chanya wa
mashabiki, walinitaka kuendelea na hiyo ilikuwa sababu ya kuendelea na kazi
yangu. Kwa upande mwingine au kwa hatua nyingine bado sijajiuzulu tena. Bado
nipo kazini kwangu na Yanga. Ni mapema sana kusema nataka kuondoka, nasema
itategemeaa na kikao nitakakachokaa na Mwenyekiti wangu”. Ameeleza Pluijm.
Mholanzi
huyo pia ametolea ufafanuzi wa kadi nyekundu aliyopata jana na kutolewa kwenye
benchi la ufundi akiwadaiwa kumsukuma mwamuzi wa mezani wa mchezo huo, Lulu
Mushi.
“Jana nilipata kadi
nyekundu kwenye mechi dhidi ya Ruvu Shooting, kwa bahati mbaya sana katika
maisha yangu ya soka niliyoanza soka la kulipwa nikiwa na miaka 17 na wakati
wote nikiwa kocha, sijawahi kupata kadi ya njano wala nyekundu. Nilishangazwa
sana nilipokwenda kumuomba mwamuzi kwamba, tafadhali unatakiwa kutenda haki kwa
timu zote, baada ya mechi meneja wangu wa timu akaniambia nilimsukuma muamuzi.
Nilienda vyumbani kwao kwasababu niliataka kujua hilo, nilimwambia kama
nimekukwaza naomba radhi, nadhani sio vizuri ukiwa kocha kupata kadi nyekundu, ni kosa langu la kwanza katika uchezaji na ukocha, lakini hakutaka
kuongea namimi, basi nikamwambia sawa, andika ripoti yako, lakini nina uhakika
mno, sijawahi kumgusa muamuzi”. Amesema Pluijm kwenye Mahojiano Maalum na MPENJA SPORTS
==
0 comments:
Post a Comment