Na Abdallah Saleh-Mdau wa MPENJA SPORTS
Mchezo utakuwa na ushindani mkubwa kwa kuzingatia ubora wa
vikosi vyote na nafasi katika msimamo wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Mtibwa Sugar inayoshika
nafasi tatu ni wazi wataingia kwenye mchezo wakitaka kukusanya alama
zote tatu ili kuendelea kujiweka mazingira mazuri zaidi.
Kwa upande wa Mabingwa Watetezi, Yanga, bila shaka wataingia Uwnajani kusaka alama tatu muhimu ili kufufua matumaini ya kuutetea ubingwa wao ambao yameingia doa kwa kutoa sare mbili na kupoteza mechi moja kati ya mitanange sita walizocheza mpaka sasa, japokuwa kimpita bado ni mapema mno.
Kiufundi Mtibwa Sugar wanaonekana kuimarika sana kwa
kiwango chao hasa katika michezo ya hivi karibuni,tofauti sana na
wapinzani wao(Yanga) ambao michezo ya hivi karibuni hawajawa
kwenye kiwango cha kuridhisha.
Mtibwa Sugar wanaotumia sana mfumo 4-4-2 na wakati fulani
4-5-1 hasa wanaposhambuliwa sana,ni wazuri katika direct play
wakichanganya na long balls na matumizi ya nguvu huku wakienda katika wide
formation wanaposhambulia.
Tatizo kubwa kwa Mtibwa linaweza kuwa kwenye
idara yao ya ulinzi, defensive pattens zao sio nzuri sana, makosa
binafsi, kushindwa kufanya pre marking imepelekea kuruhusu magoli mengi.
Idara yao kiungo imekuwa ikicheza vizuri, ni wazi watu kama Haroun Chanongo,Shabani Nditi,Kelvin Friday na Ibrahim Rajab 'Jeba' wanaweza kuwa msaada mkubwa katika mchezo huu.
Idara yao ya ushambuliaji haiko vibaya sana, lakini bado inatakiwa kuongeza umakini kwenye kutumia nafasi.
Idara yao kiungo imekuwa ikicheza vizuri, ni wazi watu kama Haroun Chanongo,Shabani Nditi,Kelvin Friday na Ibrahim Rajab 'Jeba' wanaweza kuwa msaada mkubwa katika mchezo huu.
Idara yao ya ushambuliaji haiko vibaya sana, lakini bado inatakiwa kuongeza umakini kwenye kutumia nafasi.
Kwa upande wa Yanga wanaotumia sana mfumo wa 4-4-2 angle au
4-3-3 vertical wanaweza kuwa na mabadiliko kidogo ya uchezaji hasa
kwenye idara yao ya kiungo.
Kukosekana kwa kiungo wa ulinzi wa maana
kumeifanya timu kukosa muunganiko mzuri wa kimbinu wakati wa
kushambulia. Offensively Yanga imekuwa ikimtegemea sana Thaban Kamusoko
kuandaa mashambulizi na kuchezesha timu huku akikosa backup kubwa kutoka
kiungo wa chini Technical switch ya Deus Kaseke imeonekana kufeli sana
katika michezo ya hivi karibuni,ni wazi mwalim Hans van der Pluijm anaweza akafanya
mabadiliko katika idara yake ya kiung.
Idara ya ulinzi ya Yanga bado inaonekana kucheza kwa
uelewano mkubwa, japo kidogo hupoteza umakini hasa wanaposhambuliwa sana
lakini watu kama Andrew Vicent,Vicent Bossou,Juma Abdul na Haji Mwinyi
bado ni wazuri sana kucheza kwenye eneo la ulinzi.
Idara ya ushambuliaji ya Yanga inaonekana kukosa kasi yao
ile iliyozoeleka kutokuwa kwenye kiwango bora kwa Donald Ngoma
kumeifanya kukosa nguvu kubwa ya kimbinu, ikizingatiwa huyu ndiye Play
maker kwenye idara hii, ni wazi hii ni changamoto nyingine kwa mwalimu Pluijm kuelekea katika mchezo huu.
0 comments:
Post a Comment