Mshambuliaji wa Stand United, Mnigeria, Chidiebere Abasirim, inaendelea vizuri na matibabu baada ya kupata
majeraha mabaya katika mechi ya jana ya ligi kuu soka Tanzania Bara ambayo timu
yake ya Stand United ilishinda bao moja kwa bila dhidi ya Azam FC Uwanja wa
Kambarage Shinyanga.
Chidiebere, aliruka kuwania mpira wa juu na
mlinzi wa kati wa Azam FC, Aggrey Morris ambapo Aggrey Morris alimgonga kwa kiwiko kabla ya
kuanguka vibaya .
Nyota huyo alitibiwa Uwanjani kwa dakika nyingi, lakini
jitihada ziligonga mwamba na jopo la madaktari wa Stand United wakishirikiana
na wa Azam FC walilazimika kumuondoa Uwanjani kumpeleka Hospitali kubwa kwa
matibabu zaidi.
Hata hivyo, habari zilizotufikia ni kuwa Wachezaji wa Azam
FC, wakiongozwa na kocha mkuu, Seven Hernandez wamemtembelea Chidiebere.
Miongoni mwao wanasoka hao ni Aggrey Morris aliyehusika
kwenye tukio, nahodha John Bocco, Bruce
Kangwa na David Mwantika.
Naye Kamishina wa mchezo huo, Alfred Lwiza, (Pichani kushoto) amemjulia hali Chidiebere aliyelazwa
katika Hosptali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga .
Chidiebere anaendelea na matatibabu ambapo baada ya
kufikishwa hospitalini hapo alishona sehemu aliyochanika vibaya.
0 comments:
Post a Comment