Wednesday, October 12, 2016


Na Abdallah Salehe, Mdau wa MPENJA SPORTS

MECHI nyingine kali ya Ligi Kuu Soka Tanzania Bara leo ni kati ya Stand United na Azam FC itakayochezwa kuanzia saa 10:30 Jioni Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.
Nadhani huu utakuwa mchezo wenye ushindani mkubwa na hautakuwa rahisi kwa pande zote kwa kuzingatia ubora wa vikosi na mabenchi ya ufundi ya pande zote. Pia nafasi katika msimamo wa ligi ni changamoto kubwa kuelekea katika mchezo huo.
Azam inayonolewa na kocha Mhispania, Zeben Hernandez, ni wazi itaingia uwanjani  kuziwinda Pointi tatu muhimu ili kuweza kusogea nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi, wakati Stand wao watahitaji ushindi ili kujiimarisha zaidi kwenye nafasi ya pili au kupanda kileleni kutegemeana na matokeo ya Mbeya City na Simba leo.
Stand kwasasa wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 16 baada ya kucheza mechi 8, huku Simba wakiongoza Ligi kwa alama 17 walizovuna kwenye michezo 7.
Azam inayotumia mfumo wa 4-4-2 na 4-5-1 wanaonekana kuimarika kiuchezaji,  wakicheza soka la kueleweka kuanzia mwanzo mpaka eneo la hatari la timu pinzani.
Idara ya kiungo ya Azam itatakiwa kubadilika kidogo aina yao ya uchezaji kwa kupunguza square passes ambazo kimbinu hazina madhara sana kwa mpinzani. Offensively Pattens watatakiwa kufanya kwa haraka sana ili kufika mapema kwenye attacking zone ya Stand United. 
Nafikiri mtu kama Ramadhan Singano anaweza kuwa msaada mkubwa kwenye eneo hili akicheza kama creative midfielder,  huyu anaweza kutoa option nyingi kwenye idara kiungo. Ni wazi Himid Mao atakuwa kiongozi eneo hili akicheza kama defensive midfield ikizingatiwa huyu ni ball winning midfield mzuri sana.
Sulum Abubakary ataendelea kuwepo kama central midfield akitakiwa kuichezesha timu. Licha ya uimara wa Azam kwenye safu ya kiungo, bado watatakiwa kuongeza umakini ili kuwadhibiti viungo wa Stand United.
Idara ya ushambuliaji ya Azam inaonekana kukosa umakini wa kutumia nafasi za kufunga na kucheza sana nje ya box la mpinzani na imekuwa tatizo linaloisumbua sana safu ya ushambuliaji ya timu hiyo. Hivyo katika mchezo huu watatakiwa kubadilika sana ili kuweza kuipenya ngome ya Stand. Give and go passes zinaweza kuwa na faida kwa.
Idara ya ulinzi ya Azam imeonekana kukosa muunganiko mzuri wa kimbinu, kushindwa kufanya marking kwa wakati imepelekea kuruhusu magoli mengi, hivyo watatakiwa kuongeza umakini ili kuwadhibiti washambuliaji wa Stand United ambao mara nyingi hucheza ndani ya box na kulazimisha makosa.
Kwa upande wa Stand United inayonolewa na kocha, Mfaransa, Patrick Liewig ,ni wazi wataingia katika mchezo huu kuhakikisha wanapata alama ili waendelee kusalia kujikita nafasi za juu kwenye msimamo wa lig.
Stand United inayotumia sana mfumo wa 4-4-2 wakicheza katika narrow formation ni wazuri sana kwenye half way offensive ambapo hukataa kujilinda muda wote.
Ni wazi ubora wa Stand unaanzia kwenye idara yake ya ulinzi,  watu kama Aron Lulambo, Adeyum Ahmed, Revocatus Richard na Ibrahim Isaac, wamekuwa na muunganiko mzuri kwenye idara ya ulinzi.
Idara ya kiungo ya Stand United ni sehemu ambayo viungo wa Azam watatakiwa kuwa makini sana ikizingatiwa Stand ni wazuri sana kwenye cut off,  hivyo watalazimisha kuua key players wote wa Azam. Jacob Masawe na Amri Kiemba ni wazuri sana kwa kuchezesha timu na kupiga long balls au deep Penetration passes hivyo ni watu wanaotakiwa kuchungwa sana.
Idara ya ushambuliaji ya Stand ni wazuri sana kwenye matumizi ya counter attack na mara nyingi hupenda kucheza ndani ya box ili kumlazimisha mpinzani afanye makosa,  hivyo walinzi wa Azam watatakiwa kuwa makini sana na aina hii ya mbin.
NB:
Stand United ni timu inayocheza kwa nidhamu kubwa huku fighting spirit yao ikiwa nzuri sana. Ni wazi Azam watatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kupata matokeo bora huku ubora wa sehemu ya kuchezea'pitch' ikiwa changamoto kubwa kwao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video