Thursday, October 6, 2016


Klabu ya Simba imemuomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli kutokana na uharibifu wa uwanja wa taifa uliofanywa na mashabiki wa Simba wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Yanga.
Ofisa habari wa Simba Haji Manara amesema, wanaomba radhi kwa Mh. Magufuli kwasababu ndiye anayesimamia mali zote za nchi hii kwa niaba ya wananchi wote.
“Rais wa klabu ya Simba, Kamati ya Utendaji Secretariat, benchi la ufundi na wachezaji, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba wanaomba radhi kwa Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia kwa Waziri mwenye dhamana ya michezo Mh. Nape Nnauye kwa kitendo kisicho cha kiungwana kilichofanywa na baadhi ya mashabiki wetu kwenye mchezo wa October Mosi dhidi ya Yanga.”
“Tumeona kuna umuhimu sio kumuomba radhi Mh. Waziri Nauye na TFF lakini tumeona tumuombe radhi na Rais wetu. Hizi ni rasilimali zetu zinazojengwa kwa kodi zetu, Serikali inatumia gharama kubwa kuziendesha rasilimali hizi. Ni upuuzi wa kiwango cha juu kufanya kitendo kama kile.”
“Nilishatoa taarifaya kuomba radhi mara tu baada ya mchezo ule na Rais wa klabu alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari  akiomba radhi. Tunamuomba radhi Rais wa nchi kwasababu yeye anasimamia mali za nchi hii kwa niaba ya wanachi wote.”

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video