Saturday, October 15, 2016


Na Abdallah Salehe-Mdau wa MPENJA SPORTS
 Natarajia mchezo utakuwa na ushindani mkubwa kwa kuzingatia ubora wa vikosi vya timu zote na nafasi katika msimamo wa ligi kuu ya Soka Tanzania Bara.
Simba inayoongoza msimamo Ligi ikijikusanyia alama 20 baada ya kucheza michezo 8 ni wazi itaingia katika mchezo huo kusaka alama 3 muhimu ili kuendelea kujiimarisha zaidi kileleni.
Simba inayonolewa na kocha Joseph Omog, Raia wa Cameroon inaonekana kuimarika vyema kimbinu na kiufundi.
Wakitumia mfumo wa 4-4-2 au 4-3-3 ni wazuri sana kwa kumiliki mpira huku wakifanya pressing game ili kumnyima mpinzani eneo kubwa la kushambuli.
Ubora wa Simba upo kwenye idara yake ya kiungo huku mzizi wa timu uko kwa watu kama Jonas Mkude,Mzamiru Yassin na Mwinyi Kazimoto.
 Nyota hawa wamekuwa na muunganiko mzuri wa kimbinu katika kusukuma mashambulizi na kuua mipango ya timu pinzani. Ni wazi Kagera Sugar watatakiwa kuwa makini sana na aina ya uchezaji ya viungo wa Simba.
Idara ya ushambuliaji ya simba bado inaonekana kucheza kwa utulivu mkubwa,kutokana na uimara wa kimbinu kutoka kwa viungo wao wa nyuma,muunganiko huu huwafanya washambuliaji wa Simba kuwa hatari sana kwenye eneo la mwisho,  watu kama Shiza Kichuya na Ibrahim Ajib wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kutengeneza nafasi. Fredrick Bragnon huyu ni technical aggressive,  anajua jinsi gani ya kucheza kama mshambuliaji wa kati, ni wazi walinzi wa Kagera Sugar watahitaji msaada mkubwa kutoka kwa viungo wao ili kuua muunganiko huu wa kimbinu.
Idara ya ulinzi ya simba imekuwa na muunganiko mzuri licha ya kukosa kasi kwa watu kama Method Mwanjali,Nolvaty Lufunga na Janvier Besala Bokungu, lakini uzoefu umekuwa ukiwasaidia sana kupunguza idadi ya makosa huku tatizo lao kubwa likiwa ni kushindwa kucheza mipira juu.
Kagera Sugar inayoshika nafasi ya 3 katika msimamo wa ligi hiyo ikijikusanyia alama 15 katika michezo 9 iliyocheza ni wazi itaingia katika mchezo huo kusaka alama 3 muhimu ili kujiweka mazingira mazuri zaidi.
Kagera Sugar inayonolewa na kocha Mecky Mexime mara nyingi hutumia mfumo wa 4-4-2 Diamond, nayo sio timu ya kubeza, ni wazuri sana kwenye kumiliki mpira na kujenga mashambulizi ya kasi kutokea pembeni ikizingatia kwasasa wanaonekana kuimarika kwenye pattens zao uchezaji.
Idara ya kiungo ya Kagera Sugar imekuwa na makosa ya kiufundi hasa kwenye marking,  mara nyingi huruhusu timu kushambuliwa, kushindwa kufanya pressing na kupoteza mipira kutokea katikati ya uwanja. Hii ni aina ya makosa ambayo yamekuwa yakiigharimu timu, ni wazi katika mchezo huo watatakiwa kuwa makini sana na aina ya uchezaji wa viungo wa Simba.
Idara ya ushambuliaji ya Kagera Sugar bado inaonekana kukosa muunganiko mzuri wa kimbinu kutoka kwa viungo wao, umakini kwenye kutumia nafasi ni tatizo linalo isumbua sana timu hii. Ni wazi katika mchezo huo watatakiwa kuongeza umakini ili kuweza kutumia vema nafasi zitazopatikana, matumizi ya high ball yanaweza kuwa na faida kubwa kwao kwa kuzingatia walinzi wengi hawana kasi nzuri kwenye marking.
Idara ya ulinzi ya Kagera bado kiufundi haiko vizuri sana, hushindwa kujipanga kwa wakati kufanya pre marking ni aina ya makosa ambayo yamesababisha kuruhusu magoli mengi.
Mwalimu Mecky Mexime atatakiwa kujipanga vyema safu hii ili kuweza kuwakabili washambuliaji wa Simba.
Shiza Kichuya na Ibrahim Ajib ni wachezaji wa kuchungwa sana kwenye mchezo huo,  umakini kwenye mipira ya kutengwa unahitajika sana kwa maana Simba wanaonekana ni wazuri kwa matumizi ya aina hii ya mipira.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video