Saturday, October 15, 2016

Magharibi ya Jumatano ya Oktoba 12, 2016, klabu ya Yanga kupitia akaunti yake rasmi ya mtandao wa kijamii wa Instagram, ilitoa taarifa ya kumpongeza nyota wao Simon Msuva kwa kuifungia timu hiyo bao la 50.
Bao linalozungumziwa hapo ni lile la dakika ya 69 dhidi ya Mtibwa Sugar.
Msuva mwenyewe pia kupitia akaunti yake ya Instagram, alitoa taarifa ya shukrani kwa wote walimsaidia kufikia mafanikio hayo.
Taarifa hizi zilimshtua katibu mkuu wa zamani wa klabu ya Yanga, dk. Jonas Tiboroha.
Kwa mujibu wa takwimu za Dk. Tiboroha, aliyemuibua Simon Msuva kwenye kituo chake cha WAKATI UJAO, mchezaji huyo ana mabao 53 na Yanga.
Dk. Tiboroha anasema yeye amekuwa akimfuatilia Msuva kwa sababu ni mchezaji wake aliyemlea tangu mdogo kabla hajajiunga na akademi ya Azam FC.
Kinachotia shaka zaidi ni maelezo ya Yanga kuhusu Msuva kwenye pongezi zile, klabu hiyo imesema Msuva alijiunga na Yanga 2013/14 na bao lake kwanza alilifunga dhidi ya URA ya Uganda kwenye Kagame Cup!
Swali la kujiuliza, ni Kagame gani ambayo Yanga wamecheza kuanzia 2013/14?
2013 Kagame ilifanyika Sudan na Yanga kama mabingwa watetezi hawakwenda kutetea ubingwa wao kutokana na zuio la serikali juu ya usalama.
Kagame ya 2014 ilifanyika Rwanda na Yanga hawakwenda kwa sababu ya kujichanganya juu ya kikosi cha kukitumia kwenye mashindano hayo.
Kagame ambayo Yanga ilishiriki ni ile ya 2015 ambayo Azam walikuwa mabingwa. Ina maana hapo kabla Msuva hakuwahi kufunga?
Kwa kuwasaidia Yanga, Msuva alianza kuitumikia klabu hiyo 2012/13 na bao lake la kwanza alifunga dhidi ya JKT Ruvu Sept 22, 2012. Yanga walishinda 4-1.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video