Thursday, October 6, 2016


KIKOSI cha  Mbeya City FC, 'Wana komakumwanya' kesho  kinatarajia kushuka katika uwanja wa Sokoine,Mbeya, kucheza mchezo mwingine muhimu wa Ligi kuu Soka Tanzania Bara dhidi ya wageni Stand United  kutoka mkoani Shinyanga kikiwa bila nyota wake kadhaa wa safu ya ulinzi.
Kwa mujibu wa  Ofisa  habari, Dismas Ten, maandalizi kuelekea  mchezo huo yamekamiliki na City itashuka dimbani ikiendelea kuwakosa nyota wake wawili wa safu ya ulinzi, Haruna Shamte na Sankhani Mkandawile ambao waliumia  kwenye mchezo wa ugenini dhidi ya JKT  Ruvu uliochezwa Mlandizi mkoani Pwani na City kufungwa mabao 2-0.
“Kwenye kikosi  tunaendelea  kuwakosa Haruna na Sankhani, hii  ni kwa sababu bado wanauguza majeraha lakini taarifa njema ni kuwa mlinzi Rajab Zahir amerejea  kikosini kuongeza nguvu baada ya kushindwa kumaliza dakika 90 za chezo dhidi ya Mwadui kufutia maumivu ya kifungo cha mguu, madaktari wamethibitisha kuwa yuko safi na tayari kwa mchezo wa kesho”, alisema.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video