Saturday, September 3, 2016

Licha ya kucheza kwenye uwanja wa  nyumbani, Mbao  Fc ya Mwanza  imejikuta  ikishindwa  kuhimili  vishindo vya Mbeya City Fc na kukubali kufungwa  mabao 4-1 kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania  bara  uliochezwa  leo hii kwenye uwanja wa CCM Kirumba  jijini hapa.

Mara baada ya mchezo huo kocha wa City  Kinnah Phiri, pamoja na mengine mengi lakini pia  aliwapongeza wachezaji wake kwa kucheza vizui kwa kufuata Maelekezo na hatimaye  kuibuka na ushindi  huo mnono.

“Vijana wangu wamecheza  vizuri,  wamefanya kazi kwenye kila tulichokuwa tunakifanyia mazoezi, tulijua Mbao wangekuja na mchezo wa kasi kwa sababu walihitaji sana  kushinda hasa baada ya kupoteza mchezo wao uliopita,  tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha  kupata pointi saba kwenye michezo yetu mitatu na sasa tunarudi nyumbani kujiandaa na mchzo mwingine”, Phiri alisema.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video