Monday, August 29, 2016

Chelsea wameanza vizuri mbio za kuwania ubingwa wa EPL chini ya kocha wao mpya Antonio Conte.

Wameshinda mechi zote tatu na kujikusanyia alama 9 kibindoni sambamba na Manchester City na Man United.

Lakini pamoja na yote hayo mambo si shwari kwa kiungo Cesc Fabregas ambaye ni bingwa wa kutoa pasi za mwisho.

Ujio wa N’Golo Kante ndiyo sababu kubwa ya Cesc Fabregas kukosa nafasi yake kwenye kikosi hicho kilicho chini ya Muitaliano Antonio Conte.

Hali hii imezua tetesi kwamba Muhispaniola juyo yuko mbioni kuondoka klabuni hapo huku gazeti la El Confidencial likiripoti kuwa kocha wake Conte amemuwashia taa ya kijana kuondoka klabuni hapo.

Cesc afunguka kwenye ukurasa wake wa Instagram

Baada ta tetesi hizo kuzidi mchezaji huyo wa zamani wa  Arsenal na Barcelona ameandika haya kwenye Instagram yake.

"Contrary to what has been written, the manager and I have a good relationship and he has NEVER told me that I can leave. He said that he counts on me, as I count on him. I will continue to fight for this club until the very end and when called upon I will always give my very best. I'm fully committed to @chelseafc and my only goal is to help them win more trophies. #ChelseaFC"

"Kinyume na ambavyo imekuwa ikiandikwa, uhusiano wangu na meneja ni mzuri na kamwe hajawahi kuniambia kwamba naweza kuondoka klabuni. Alichokisema ni kwamba bado ananihesabia, kama ambavyo mimi namhesabia pia. Nitaendelea kupambana kwa kila hali mpaka mwisho, na meneja atakaponipa nafasi nitapambana kwa juhudi zangu zote. Bado nina moyo ule ule wa kujitolea klabuni hapa@chelseafc na lengo langu kuu ni kuhakikisha naisaidia timu kushinda mataji mengi zaidi. #ChelseaFC"

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video