Tuesday, August 16, 2016

Timu ya soka ya Yanga imeendelea na programu zake za mazoezi kwaajili ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam utakaopigwa kesho Jumatano katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaa.
Mchezo wa Ngao ya Jamii huashiria ufunguzi wa msimu mpya. 
Katika mchezo huo, Yanga inaenda kushuka dimbani, huku ikitarajiwa kuwakosa nyota wake kadhaa kutokana na kusumbuliwa na majeraha yaliyotokana na michezo yao ya Kombe la Shirikisho.
Wachezaji ambao wanatarajiwa kukosekana ni pamoja na Ally Mustafa ‘Barthez’ anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu (ankle), mabeki Juma Abdul, Andrew Vincent ‘Dante’ wanaosumbuliwa na maumivu ya miguu.
Wengine ni Kevin Patrick Yondani anayesumbuliwa na maumivu ya jicho na kiungo mshambuliaji Obrey Chirwa anayesumbuliwa na goti.
Mshambuliaji tegemezi wa timu hiyo Mzimbabwe Donald Ngoma anarudi uwanjani baada ya kukosekana kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya MO Bejaia kutokana na kuwa na kadi mbili za njano.
Yanga ambao pia walikuwa wakisaka tiketi ya kufuzu nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika wametupwa nje baada ya Medeama kuifunga TP Mazembe kwenye mchezo uliopigwa nchini Ghana juzi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video