Arsenal imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Man City iliyopigwa jana usiku.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Theo Walcott, Alex Iwobi na Chuba Akpom.
Wakati mawili ya Man City yalifungwa na Kun Aguero na Kelechi Iheanacho.
Hata hivyo, Arsenal bado wamezidi kupata balaa katika safu yao ya ulinzi kuelekea mechi ya ufunguzi wa ligi kuu England dhidi ya Liverpool baada ya beki Gabriel kutolewa jana kwa machela kufuatia kupata majeraha.
Hii inamaanisha Arsene Wenger hatakuwa na beki yeyote mzoefu wa kati kwenye kikosi chake mwanzoni mwa Msimu.
Per Mertesacker yuko nje ya dimba kwa miezi minne, wakati Laurent Koscielny bado hajarejea mazoezini.
Vijana Ron Holding na Calum Chambers ndio pekee wapo salama kikosini mpaka sasa.
0 comments:
Post a Comment