Pogba. Kiungo wa Kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23, aliwasili Jijini Manchester mapema jana ili kuanza kukamilisha Uhamisho wake kutoka Juventus ya Italy kwa Dau la Rekodi ya Dunia la Pauni Milioni 89.
Kutoka Uwanja wa Ndege wa Manchester, Pogba alibebwa na Gari Nyekundu ya Kifahari aina ya Chevrolet ambao ni Wadhamini rasmi wa Man United.
Kufuzu Afya kwa Pogba sasa kunaachia wazi leo Jumanne kutangazwa kwake kuwa Mchezaji Mpya wa Nne kununuliwa na Man United katika kipindi hiki chini ya Meneja Mpya Jose Mourinho ambae Juzi aliiongoza Man United kutwaa Ngao ya Jamii baada ya kuwachapa Mabingwa wa England Leicester City 2-1 huku Bao la ushindi likifungwa na Straika mpya 'Mjivuni' Zlatan Ibrahimovic.
Wachezaji wengine wapya wa Man United ni Eric Bailly na Henrikh Mkhitaryan.
0 comments:
Post a Comment