MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri kuogopa kustaafu na haelewi ni kwa namna gani makocha kama Sir Ferguson wameweza kuendena na maisha ya baada ya soka.
Wenger ambaye amekuwa akiifundisha Arsenal karibia miaka 20 sasa, mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu, lakini kocha huyo mwenye umri wa miaka 66 haonekani kama yuko tayari kustaafu ambapo anasema mapenzi aliyonayo kwenye mchezo wa soka, hayaelezeki.
"Imekuwa ni maisha yangu, kiukweli, naogopa siku itakapofika (kustaafu)". Wenger amekiri hilo.
Wenger anatarajia kuiongoza Arsenal msimu wa 2016/2017 kusaka ubingwa wa nne wa ligi kuu ya England, lakini bado hatumii fedha nyingi kuimarisha kikosi chake wakati huu wa usajili wa majira ya kiangazi.
0 comments:
Post a Comment