Paris Saint-Germain imetangaza kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Jese Rodriguez kwa dau la paundi milioni 21.2.
Mchezaji huyo mwenye miaka 23 alibakiza mwaka mmoja Berbabeu, lakini amechagua kutimkia Paris ambapo amesaini mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ufaransa.
Timu za Arsenal na Liverpool zilikuwa zikihusishwa kuiwania saini ya straika huyo, lakini ameungana na kocha mpya wa PSG, Unai Emery na ni usajili wa tano kwa kuocha huyo majira haya ya kiangazi.
Jese amepewa jezi namba 22.
Baada ya kukaa miaka 9 ya Mafanikio Real Madrid, Jese ameunga na Hatem Ben Arfa, Grzegorz Krychowiak, Thomas Meunier na Giovani Lo Celso katika dimba la Parc des
Baada ya ku-post picha akiwa na mpenzi wake, Aurah Ruiz , Jese amezungumza na Tovuti ya PSG kuelekezea usajili wake.
"Nimefurahi sana kujiunga na Paris Saint-Germain, ambayo imekuwa miongoni mwa klabu zenye ushindani mkubwa barani Ulaya," Amesema Jese.
0 comments:
Post a Comment