Kuelekea msimu mpya wa Ligi kuu ya soka ya Hispania, Laliga, Lionel Messi na Luis Suarez wameonesha makali yao ya kufumania nyavu wakiiwezesha Barcelona kushinda 3-2 dhidi ya Sampdoria katika mechi ya kombe la Gamper.
Messi alifunga mabao mawili na moja lilifungwa na Suarez.
Tazama wafungaji wa timu zote hapa chini na vikosi vyao:
Mechi hiyo ya Joan Gamper Trophy ni ya kirafiki ya kila mwaka ikihodhiwa na Barcelona kwenye uwanja wa Camp Nou na inachezwa mwezi wa nane kila mwaka kabla ya Barca kuanza msimu mpya wa Laliga.
Mchezjo huo umepewa heshima ya Joan Gamper ikiwa ni sehemu ya kumuenzi gwiji huyo ambaye ni muanzilishi, akawa mchezaji wa timu hiyo na baadaye Rais wa klabu ya Barcelona.
Mashindano hayo yalifunguliwa mwaka 1966 na Enric Llaudet ambaye alimrithi Gamper katika nafasi ya Urais.
0 comments:
Post a Comment