Eliaquim Mangala hayupo kwenye mipango ya kocha Guardiola |
Wakati Dirisha la usajili wa majira ya Joto likitarajiwa kufungwa mwishoni mwa mwezi huu, Pep Guardiola bado anaangaza macho kutafuta wachezaji wengine wanaoweza kuimarisha kikosi chake cha Manchester City.
Mpaka sasa Guardiola ameshatumia karibia paundi milioni 90 kusajili wachezaji tangu awasili Etihad, lakini sasa nguvu zake zipo kwa John Stones wa Everton ambaye wiki hii anaweza kukamilisha usajili wake.
John Stones |
Mlinzi huyo wa Everton anaweza kuwa mchezaji wa sita kusaini timu kubwa ya Man City, huku akimuacha njia panda Guardiola ambaye atalazimika kutafuta wanunuaji kwa wachezaji wake Wilfried Bony, Samir Nasri, Jesus Navas na Eliaquim Mangala.
Pep Guardiola anapanga kuuza baadhi ya wachezaji |
Guardiola anaamini nafasi ya Mangala itazibwa na Stones, lakini Everton hawana presha ya kumuuza na wanagoma kuchukua dau la paundi milioni 50.
Guardiola ana hali ngumu kwenye safu yake ya ulinzi kutokana na Vincent Kompany kutokuwa fiti, huku Nicolas Otamendi naye akiwa majeruhi.
Tosin Adarabioyo ndiye ameonekana kuwa chaguo la kwanza katika mechi ya Jumamosi ya EPL dhidi ya Sunderland na hii imetokana na skuoneha kiwango kizuri wakati wa maandalizi ya msimu mpya.
Wilfried Bony hana chake sasa Man City
Guardiola amesema Nasri amekuwa na uzito mkubwa baada ya kurejea akitokea mapumzikoni
0 comments:
Post a Comment