Thursday, August 11, 2016

Mchana wa leo zimeripotiwa Taarifa za Mshambuliaji Mkongwe wa klabu ya Simba, Musa Hassan Mgosi kustaafu rasmi soka na kupewa nafasi ya Umeneja wa klabu hiyo.
MPENJA SPORTS imemtafuta Mgosi na kumuuliza juu ya taarifa hizo na maelezo yake ni haya: “Kwanza napenda kukanusha suala lililoandikwa kwenye mitandao la Mgosi kustaafu, Mgosi kama Mgosi, suala la kustaafu mpira bado sana, Pogba (Paul) atakapostaafu ndipo atafuatia Mgosi kustaafu”. Amesema Mgosi na kuongeza”

Hata hivyo, Mgosi ameonesha wazi yuko tayari kufanya kazi yoyote ndani ya Simba hata kama atakuwa nje ya uwanja, kitu kinachoashiria yuko mbioni kutundika daluga.

 “Mimi ni mchezaji wa Simba, ni Mfanyakazi wa Simba, nipo tayari kufanya majukumu yoyote yanayoihusu Simba, aidha katika uchezaji au sekta nyingine”.

Mgosi anayeheshimika ndani ya Simba amesema kutekeleza majukumu mengine nje ya kucheza ndani ya Simba alishaanza msimu uliopita, lakini hakuna aliyehusisha na kustaafu soka.

“Kuisaidia Simba nje ya uwanja nimelifanya hilo toka mwaka jana, lakini mbona halijaandikwa hivyo, mwaka jana nimekuwa msaidizi wa Mayanja (Jackson), nilimsaidia kila kitu kama kocha msaidizi”. Amesisitiza Mgosi na kufafanua: “Unapozungumza mtu kistaafu tuwe na subira, lazima niseme mwenyewe, sio mitandao iandike, wengine wanaandika wapate comments, likes na kushtusha watu ambao wananihitaji.”

MPENJA SPORTS imemuuliza kama anaamini muda wa kustaafu umefika na yuko tayari kuwa Meneja wa Simba.

 “Sio tatizo,  ni jukumu ambalo nitalifanyia kazi kwa vile ninavyofahamu mimi, ukitaka kuangalia kiongozi anayeweza kuingoza Simba kwa kila kitu, hakuna mtu ambaye kwa haraka unaweza kumuangalia zaidi ya Mgosi,  kwasababu ni mtu ninayeheshimika na wachezaji, naheshimika na mashabiki, naheshimika na viongozi wa Simba, naamini katika sekta yoyote nitakayopewa Simba, hakuna atayepinga, kwahiyo najivunia klabu yangu ya Simba.”. Ameongeza Mgosi.

Licha ya kakanusha kustaafu rasmi, taarifa za ndani ambazo MPENJA SPORTS imezipata ni kuwa kweli Mgosi anaelekea kustaafu na mechi ya Jumapili dhidi ya URA itakuwa maalum kwake kuagwa, lakini yeye mwenyewe na uongozi hauko tayari kulizungumzia kwasababu kuna masuala kadhaa wanajadiliana.


Inaelezwa keshokutwa Jumamosi, Mgosi atakutana  na viongozi wa Simba kujadili suala la nafasi wanayotaka kumpa ikiwemo kuandaa mkataba .

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video