Thursday, August 18, 2016

Barcelona usiku wa kuamkia leo wakiwa katika dimba lao la Nou Camp wamiaidhibu Sevilla 3-0 na kutwaa ndoo ya Supercopa de Espana baada ya kuwa na wastani wa mabao 5-0, kufuatia mechi ya kwanza kushinda magoli 2-0.
Waliowapa furaha mashabiki wa Barcelona ni Arda Turan aliyefunga mabao mawili, pamoja na Lionel Messi aliyeingia wavuni mara moja.

Hii inakuwa mara ya kwanza kwa Wakatalunya hao kutwaa ubingwa huo tangu walivyofanya hivyo mara ya mwisho mwaka 2013.

Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Barca walikuwa mbele kwa 1-0 lililofungwa dakika ya 10 na Arda Turan.

Arda aliongeza lingine dakika ya 47 kabla ya Messi kushindilia msumari wa mwisho dakika ya 56 

Supercopa de Espana ndio Mechi ya kufungua pazia Msimu mpya wa Spain na hushindaniwa na Bingwa wa La Liga na aliebeba Copa del Rey lakini Msimu uliopita Barca, chini ya Kocha Luis Enrique, walibeba vyote na hivyo Sevilla kuwakilisha kwa vile wao ndio walifungwa Fainali ya Copa del Rey.

Barca na Sevilla zitaanza Msimu mpya wa La Liga Jumamosi kwa Barca kucheza Nyumbani na Real Betis wakati Sevilla pia wakiwa Nyumbani kucheza na Espanyol.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video