Shkodran Mustafi |
Kuelekea
msimu mpya wa ligi kuu soka ya England, Arsenal wapo kwenye wakati
mgumu katika safu yao ya Ulinzi baada ya kuumia kwa Gabriel na hali hiyo
imeanza kumtisha zaidi kocha Arsene Wenger wakati huu anajiandaa
kufungua dimba la EPL dhidi ya Majogoo wa Jiji Liverpool, Jumapili ya Juma hili.
Gabriel
aliumia katika mechi ya kirafiki iliyochezwa jana kati ya Arsenal na
Manchester City na kushuhudia Washika Bunduki hao wa London wakiibuka na
ushindi wa mabao 3-2.
Hata
hivyo taarifa zinasema kuumia kwa Mbrazil huyo kumeongeza juhudi kwa
Wenger kuisaka saini ya mlinzi wa Valencia Shkodran Mustafi kwa dau la
paundi milioni 40.
Mjerumani
huyo ni Mlinzi chaguo namba moja la Wenger katika mipango yake ya
usajili majira haya ya kiangazi na alipoulizwa kama atamsajili, amejibu: "Nimeshalisema mara
nyingi sana, tuko sokoni. Kiukweli sio soko rahisi kwetu, tuamini habari
njema zitakuja".
0 comments:
Post a Comment