Mashabiki wa England wamelazimika kukimbia na kutoka nje ya baada ya kuvamiwa na mashabiki wa Urusi kwenye uwanja wa Stade Velodrome baada ya mchezo kati ya pande hizo mbili kumalizika kwa sare ya 1-1 mjini Marseille.
Muda mfupi tu baada ya kumalizika kwa mchezo, ambapo Glushakov alifunga bao la kusawazisha katika dakika za majeruhi, mashabiki wa Urusi walivamia jukwaa la mashabiki wa England ambao walilazimika kupanda uzio ili kukimbia.
Kwa siku ya tatu mfululizo mashabiki wa pande hizi mbili wamekuwa wakikabiliana.
0 comments:
Post a Comment