Wednesday, May 25, 2016

Ubingwa usiotarajiwa wa Leicester City unaweza kuwa umewafanya wawe maarufu zaidi duniani lakini Arsenal ndio timu iliyopata fedha nyingi zaidi msimu huu kwenye EPL.

Takwimu rasmi zilizochapishwa leo Jumanne zinaonyesha Gunners wameingiza kiasi cha £101million – kutoka kwenye mapato ya Premier League.

Manchester City wameshika nafasi ya pili katika listi waliopata hela nyingi – wakiingiza £96,971,603, wakifuatiwa na Manchester United (£96.5m) na Tottenham (£95.2m), huku mabingwa Leicester wakishika nafasi ya tano kwa kuingiza £93.2m. Timu iliyoingiza fedha chache zaidi ni Aston Villa, walioingiza £66.6m, fedha nyingi zaidi kuwahi kupokea timu iliyoshika nafasi ya mwisho kwenye ligi.

Fedha hizi kwa asilimia kubwa zinatoka kwenye dili kubwa la haki ya matangazo ya TV lakini pia kutoka kwenye mapato ya jumla ya kibiashara kwa kila klabu.

Fedha walizoingiza Arsenal zina mchanganuo ufuatao – £23,605,000 zilitokana na kumaliza nafasi ya pili kwenye ligi, £21,496,762 zimetokana na mauzo ya haki za TV – Gunners mechi zao nyingi zilioneshwa live, pamoja share nyingine ya dili ya kuonyesha mechi kwenye TV za ndani na kipato kingine cha matangazo ya biashara ya wadhamini wa ligi kaka vile Barclays.

Kila klabu baada ya hapo inapokea kiasi cha
£1,242,405 kulingana na kila nafasi waliyoshika kwenye ligi – kuanzia chini kwa Aston Villa mpaka mabingwa Leicester waliopata kiasi cha £24,848,100. Kila klabu pia hupata kiasi cha fedha kwa kutegemea mara ngapi wameonyeshwa mechi zao live katika Sky au BT. Kila klabu inapata kiasi cha wastani wa chini wa £8,782,088 kutoka katika mgawanyo huu, hata kama wakionyeshwa mara chache kama Watford na Bournemouth ambao mechi 8 kila timu ilipata kuonyeshwa live – Norwich City na Stoke City (mara 9 kila timu).

Arsenal walionyeshwa live UK zaidi, mara 27, wakifuatiwa na Manchester United 26 halafu City 25, Liverpool 23, na Chelsea 22.

Kwa msimu wa 2015-16 kila klabu ilipata mgawo sawa wa £55,849,800 kutokana na mapato ya kuonyeshwa mechi zao nyumbani, mapato ya nje na mapato ya kibiashara.
Vilabu vina vyanzo vikuu vitatu kwa kuingiza fedha: Mauzo ya mechi (tiketi, mauzo ya nafasi pekee za watu mashuhuri) mapato kutoka kwenye vyombo vya habari ambayo ndio makubwa zaidi pamoja na mapato ya kibiashara (dili za vifaa , udhamini, mauzo ya malighafi mbalimbali, ziara na vitu vingine).
Sky na BT Sport walilipa kiasi cha £3.018billion ili kupata haki za kuonyesha mechi live nchini Uingereza kwa miaka 3 kutok 2013 mpaka 2016. Vyombo vya habari vya nje wakalipa kiasi kingine cha £2.23bn kwa kipindi hicho ili kuonyesha EPL live nje ya UK. Fedha za zawadi zitakuwa nyingi kuanzia msimu ujao. Dili za haki za kuonyeshamechi Uk zitapanda kutoka £3.018bn mpaka £5.136bn kuanzia msimu ujao mpaka 2019, na mauzo ya nje yatapabda kutoka £2.23bn mpaka £3bn.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video