Thursday, May 26, 2016


Arsenal tayari wamethibitisha kumsajili kiungo wa Borussia Monchengladbach Granit Xhaka kwa ada inayokadiriwa kufuka paundi milioni 30.
Mswizi huyo atakuwepo katika michuano ya EURO 2016 huko nchini Ufaransa na atajiunga na Arsenal punde tu baada ya michuano hiyo kumalizika.
“Ninajivunia sana kujiunga na Arsenal,” alisema Xhaka. “Ninasubiri kwa hamu sana kuungana na wenzangu kuiwakilisha timu yetu katika michuano mbalimbali hasa ligi kuu. Ninajitoa kwa kila hali kuhakikisha kuwa naipa makombe Arsenal na kuwafanya mashabiki kuwa na furaha.”
Kwa upande wake kocha Arsene Wenger amesema: “Granit Xhaka ni mchezaji kijana na mwenye uwezo wa hali ya juu, na kitu kizuri zaidi tayari ana uzoefu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na ligi ya Bundesliga.
“Tumekuwa tukimwangalia kwa muda mrefu sana kwa hiyo ni mchezaji ambaye tunatarajia ataongeza ubora katika kikosi chetu. Tunamtakia Granit kila la heri katika Euro 2016 akiwa na taifa lake la Uswizi na tunamngoja kwa hamu kuungana na wenzake pindi michuano hiyo itakapomalizika kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.”

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video