Friday, September 4, 2015

SAID Ndemla na Ibrahim Ajib ni miongoni mwa wachezaji wa Simba waliopo katika kikosi cha Taifa Stars ambao kesho watabadili msimamo wa mashabiki wa Yanga kwa kuwashangilia watakapoivaa Nigeria kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba na Yanga zenye upinzani wa jadi zimekuwa na uhasama wa muda mrefu ambapo zimekuwa hazitakiani heri mojawapo inapocheza na timu nyingine.
Uhasama baina ya timu hizo umekuwa ukiendelea hata kwa wachezaji mmoja moja hata pale anapokuwa katika majukumu ya timu ya Taifa.
Mathalani, mchezaji wa Yanga aliyepo Taifa Stars anapoboronga au kutolewa wakati timu hiyo inapocheza na timu yoyote, huzomewa mno na mashabiki wa Simba.
Hali huwa hivyo pia kwa mchezaji wa Simba anapofanya vibaya akiwa Stars kwa kujikuta katika wakati mgumu mbele ya mashabiki wa Yanga.
Lakini katika kile kinachoonekana mashabiki wa soka Tanzania kufahamu maana na neno ‘kuweka silaha chini’, wale wa Yanga wametangaza rasmi kuweka kando uhasama wao wa jadi na Simba kwa kuwashangilia wachezaji wa Wekundu wa Msimbazi hao waliopo Stars katika mchezo wa kesho.
Wakizungumza na BINGWA Dar es Salaam jana, mashabiki hao walisema wana kila sababu ya kwenda kwa wingi Uwanja wa Taifa kuishangilia Stars, wakisisitiza kuonyesha uzalendo wa hali ya juu kuishangilia Stars inayonolewa na mzalendo, Charles Boniface Mkwasa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video