Monday, July 6, 2015


Na Ramadhani Ngoda.
Wakala wa Mlinda mlango wa klabu ya Real Madrid na timu ya tifa ya Hispania, Iker Casillas, Carlo Cutropia ameweka wazi kuwa mteja wake anataka kutimkia kunako klabu ya Porto inayoshiriki ligi kuu nchini Ureno anakoona atapata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza.

“Casillas anavutiwa na ana shauku na kujiunga na Porto,” alisema wakala huyo kukiambia chombo kimoja cha habari.

Nafasi ya mlinda lango huyo imekuwa mashakani baada ya Madrid kuwa mbioni kunasa saini ya mlinda lango wa Manchester United, David De gea anayeonekana kuwa wake mbadala sahihi Santiago Bernabeu.

Casillas (34) aliyeichezea Madrid Zaidi ya michezo 700 (katika mashindano yote) tangu alipoingia rasmi kwenye kikosi cha kwanza msimu wa 1999/2000, ana Imani kuwa klabu hiyo itamfungulia mlango wa kutokea na kumpa Baraka zote aendapo.

“Tuna Imani Madrid watamruhu kuondoka bila shaka yoyote,” aliongeza wakala huyo.

Casillas anafikia uamuzi wa kuondoka Madrid licha ya kuwa na kandarasi na miamba hiyo ya Hispania mpaka Juni 2017.

Mpaka sasa amekwisha shinda mataji 5 ya La Liga, mataji 2 ya Copa Del Rey, pamoja na kushinda Super copa De Espana mara 4 bila kusahau ligi ya mabingwa Ulaya alioshinda mara 3, Super Cup mara 2 na kombe la dunia kwa vilabu (FIFA Club world cup).






0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video