Monday, July 6, 2015

Johan Cruyff, Uholanzi (1966-77: Mechi 48 magoli 33)
Alishinda mataji mengi akiwa na klabu ya Ajax, Barcelona na Fayenood, lakini hakuwahi kutwaa taji hata moja akiwa na timu ya taifa ya Uholanzi. Alishinda makombe 10 kwenye ngazi ya vilabu lakini mkongwe huyo alishindwa kutwaa kombe lolote kwenye timu yake ya taifa.
Uholanzi ilikuwa mshindi wa pili kwenye kombe la Dunia lililofanyika Ujerumani nMagharibi mwaka 1994 na wenyeji wakatwaa kombe na Uholanzi ikashika nafasi ya tatu kwenye michuano ya Euro mwaka 1976 nchini Yugoslavia.
Ferenc Puskas, Hungary (1945-55: 85 Mechi, magoli 84), Hispania (1961-62: Mechi 4 , magoli 0)
Hungary ilitawala mchezo wa soka miaka ya 1950. Puskas kama ilivyo kwa Messi, alishinda medali ya dhahabu kwenye michuano ya Olympic 1952 na hawakupoteza hata mmoja kwa kwa miaka minne mpaka wanacheza michuano ya kombe la dunia mwaka 1954.
Walifika hatua ya fainali na Puskas alifunga goli kwenye mchezo huo lakini baade walichezea kichapo cha goli 3-2 na Ujerumani Magharibi na kupoteza mchezo huo. Puskas aliweka historia ya kufunga magolin 84 kwenye mechi 85 alizocheza akiwa na timu yake ya taifa.
Eusebio, Ureno (1961-73: Mechi 64, magoli 41)
Aliweza kuandika historia kubwa kwenye mchezo wa soka wa kutwaa mataji 11 na taji moja la Ulaya akiwa na klabu ya Benfica.
Mshindi huyo wa Ballon d’Ormwaka 1965 alikaribia kucheza fainali ya kombe la dunia wakti timu yake ilipomaliza nafasi ya tatu kwenye michuano hiyo ya kombe la dunia ya mwaka 1966.
Zico, Brazil (1976-86: 71 Mechi, 48 magoli)
Tuzo alizoshinda kama mchezaji binafsi ni nyingi. Ni mchezaji ambaye aling’ara mwishoni mwa miaka ya 1970 na mwanzoni mwa 1980, ambapo Pele alishawahi kumtaja kuwa ni miongoni mwa wajezaji bora duani. 
Zico alishuhudia Brazil ikimaliza nafasi ya tatu kwenye kombe la dunia la mwaka 1978 na aliifikisha robo fainali mwaka 1986 lakini kamwe hakutwaa ndoo akiwa na Brazil.
Paolo Maldini, Italy (1988-2002: Mechi 126, magoli 7)
Maldini alishinda vikombe saba vya ligi ya Italia (Serie A) akiwa na AC Milan vikombe vitano vya kombe la Ulaya, lakini alipokuwa akiichezea timu ya taifa hakuambulia kitu.
Italia ilikuwa mshindi wa pili kwenye kombe la dunia la mwaka 1994 pamoja na Euro mwaka 2000, huku ikiambulia nafasi ya tatu kwenye michuano ya kombe la dunia mwaka 1990 na nusu fainali kwenye michuano ya Euro mwaka 1988.
Maldin alitundika daruga akiwa na umri wa miaka 34 baada ya kombe la dunia la mwaka 2002 na miaka minne baadae Italy ikabeba ndoo ya dunia mwaka 2006.
Roberto Baggio, Italy (1988-2004: Mechi 56, magoli 27)
. Mchezaji mwingine wa Italy aliyeisaidia timu yake kwenye fainali za kombe la dunia mwaka 1994 na kumaliza akiwa mfungaji bora wakati wa kuwania nafasi ya kushiriki michuano hiyo. 
kibaya zaidi ni kwamba baada ya mchezo kumalizika kwa sare ya 0-0 ikabidi mshindi atafutwe kwa mikwaju ya penati. Baggio akakosa penati yake na kuwaacha Brazil watwae kombe.
Michael Ballack, Ujerumani (1999-2010: Mechi 98, magoli 42)
Ballack aliifikisha Ujerumani kwenye fainali ya kombe la dunia mwaka 2002 lakini hakucheza mchezo wa fainali kufuatia kulimwa kadi kwenye mchezo wa nusu fainali dhidi ya Korea Kusini.
Kwenye mchezo wa fainali Ujerumani iliishia kuambulia kichapo cha goli 2-0 na Brazil kunyakua kombe hilo, mwaka 2008 akaipeleka tena Ujerumani kwenye mchezo wa fainali ya Euro lakini kama kawaida hawakufua dafu mbele ya Hispania baada ya kulazwa kwa goli 1-0.
Katika kumbukumbu mbaya za mchezaji huyo, Ballack hajawahi kushinda taji lolote kubwa ukiahilia mataji ya ligi.
Paul Gascoigne, England (1988-98: Mechi 57, magoli 10)
Sure, you could name other England icons such as Ukitaja nyota wa England kama David Beckham, Steven Gerrard, Paul Scholes, hata George Best, lakini huwezi kuacha kulitaja jina la Gascoigne. 
Ilikuwa ni mwaka 1990 ambapo Engand ilimaliza nafasi ya nne lakini Gascoigne alipewa kadi ya njano iliyomaanisha asingecheza mchezo wa fainali kitu kilichomfanya amwage machozi.
Michael Laudrup, Denmark (1982-98: Mechi 104, magoli 37)
Laudrup alikuwa nyota aliyeshinda mataji akiwa na Juventus, Barcelona, Real Madrid na Ajax.
Lakini hakuweza kushinda kombe lolote akiwa na Denmark. Walishinda izuri kwenye Kundi E kwenye michuano ya kombe la dunia la mwaka 1986 lakini wakachezea kichapo cha goli 5-1 mbele ya Hispania.
Na wakati Denmark inashinda kombe la mataifa ya Ulaya mwaka 1992, Laudrup alikuwa tayari ameshastaafu soka.
Cristiano Ronaldo, Ureno (2003-hadi sasa: Mechi 120 , magoli 55)
Muda unazidi kuyoyoma kwa mchezaji huyo mwenye miaka 30 ambaye hataki kutundika daruga bila kutwaa taji lolote ili aongezee kwenye CV yake inayokosa kombe akiwa na timu yake ya Ureno.
. Ronaldo asingekuwepo kwenye orodha hii, lakini fainali ya Euro mwaka 2004 ambayo Ugiriki iliifunga Ureno na kutwaa kombe lhilo la mataifa ya Ulaya.
Je, Messi au Ronalo wanaweza kutwaa mataji wakiwa na timu zao za Taifa? Muda unazikdi kwenda kasi sana kwa wote wawili.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video