Monday, July 27, 2015

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, barua aliyoandika kocha wa zamani wa Liverpool, mwenye historia kubwa, BILL SHANKLY akiomba kustaafu mwaka 1974 imeonekana.
Akiaminika kuwa ndiye kocha mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika soka la England, Shankly aliyefariki dunia  mwaka 1981 akiwa na miaka 68 aliifundisha Liverpool kwa mafanikio katika kipindi cha miaka 15 kabla ya kustaafu.

Nyaraka hiyo imefichuliwa na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, JOHN ALDRIDGE katika maktaba ya HOTELI YA SHANKLY na baada ya hapo akaandika kwenye mtandao wake wa Twitter akisema hii ndio barua aliyoandika akiomba kustaafu.

Barua hiyo aliyoandika Juni 18, 1974 iliwasilishwa kwa mwenyekiti wa Liverpool wa wakati huo, JOHN SMITH akisomeka kwamba , SHANKLY anaomba kustaafu kuifundisha Liverpool  haraka iwezekanavyo na litakuwa jambo zuri kama klabu hiyo itaanza kuandaa mafao yake.

Maombi hayo yalikubaliwa na Smith Julai 12 mwaka huo ambapo aliitisha mkutano na waandishi wa habari akisema kuwa Liverpool imepokea maombi ya ya kujiuzulu kwa kocha wao na bodi ya klabu imekubali, huku akimshukuru kwa mchango mkubwa aliotoa Anfield.


SHANKLY, aliyeanza kuifundisha Liverpool mwaka 1959, alishinda makombe matatu ya ligi daraja la kwanza, mataji mawili ya FA na komba la UEFA, huku akiifanya Liverpool itawale soka la England miaka ya 70 na 80.

Bill Shankly's letter of resignation as Liverpool manager, penned in 1974, has been revealed forty years later

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video