Friday, July 31, 2015

MWAKA 2012, Azam FC waliweka rekodi ya kuingia Fainali ya kombe la Kagame wakiifunga 2-1 AS Vita Club ya Congo DR katika mechi ya nusu fainali iliyopigwa uwanja wa Taifa,  Dar es salaam.
Wakati huo ikiwa ni takribani miaka sita tu tangu kuanzishwa kwake, Azam iliweza kuiondoa klabu kongwe ya AS Vita ambayo inatikisa soka la DR Congo na iliwahi kushinda kombe la Afrika mwaka 1973.
Msimu mmoja kabla ya kukutana na Azam katika mechi hiyo, AS Vita walichukua ubingwa wa Congo DR wakiwashinda wapinzani wao wakubwa, TP Mazembe ambao walikuwa mabingwa wa Afrika 2009 na 2010.
Kipute hicho cha nusu fainali kilikuwa kikali mno ambapo AS Vita walianza kufunga goli la kuongoza dakika ya 35 kupitia kwa Alfred Mfongang  akiachia shuti kali umbali wa mita 30 kutoka kwenye eneo la hatari kufuatia kumzidi maarifa mlinzi wa Azam, Said Mourad.

Dakika ya 39, beki wa AS Vita, Issama Mpeko alionyeshwa kadi ya pili ya njano. Tukio hili lilikuwa baya kwa mwamuzi wa kati, Dennis Batte kutoka Uganda kwani alishindwa kugundua kwamba Mpeko alitakiwa kupewa kadi nyekundu.

Mpeko alicheza kwa dakika tatu kabla ya Batte kugundua kwa msaada wa waamuzi wasaidizi.

Licha ya kufungwa goli hilo, Azam walikuwa na matumaini ya kusawazisha na hawakubweteka kwasababu wapinzani wao wamebaki 10. Walijua wana dakika nyingine 45 za kuandika rekodi.

Erasto Nyoni alipiga krosi maridadi ambayo ilimaliziwa kwa kichwa na Nahodha John Bocco akiisawazishia Azam dakika ya 68.

Dakika mbili baadaye, Azam walifunga goli lingine la kichwa kutokana na mpira wa kona, lakini mwamuzi alilikataa  akidai golikipa Nelson Lukong amesukumwa.


Azam waliendeleza mashambulizi langoni mwa Vita na kwa mara ya kwanza katika mashindao ya mwaka huo, Wacongo walionekana kubanwa tofauti na mechi zote walizocheza kuanzia hatua ya makundi.

Licha ya kukaza kwa zaidi ya saa ya mchezo, dakika ya 88,  Mrisho Ngassa aliwaacha mabeki wa Vita na kuiwahi pasi ya Abubakar Salum 'Sure Boy' na kuandika bao la pii.

Kocha wa AS Vita , Medard Lusadisu alikubali kushindwa na akalisifu soka la ukanda wa Afrika mashariki na kati.

Hakuweza kujitetea kwasababu ya kadi nyekundu akisema: "Ukipata kadi ya pili ya njano unatolewa kwa kadi nyekundu, ndivyo ilivyo. Tumejifunza mengi kutoka mpira wa CECAFA, upo kiwango cha juu sana".

Kumwagiwa sifa na klabu maarufu ya AS Vita inayopambana na timu zilizofanikiwa katika soka la Afrika kama vile TP Mazembe, DC Motema Pembe lilikuwa jambo la faraja kwa CECAFA.

Kocha wa Azam fc, Stewart Hall alisema ni mafanikio makubwa kufika fainali.

"Wamiliki wa timu hii (Azam fc) wanataka kuweka historia katika soka na biashara kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati pamoja na Afrika nzima. Nadhani sisi watu wa mpira tupo njia sahihi kuwasaidia kufanikisha nia yao"

Kocha huyo aliyekuwa na furaha alisema anaangalia mechi ya fainali ambapo alimsubiri mpinzani kutoka katika mechi ya waliokuwa mabingwa watetezi, Yanga dhidi ya APR kutoka Rwanda.

Stewart alisema: "Sitaiangalia mechi hiyo! sijali nani atashinda".

Yanga walishinda 1-0  dhidi ya APR, goli likifungwa na Hamis Kiiza dakika ya 100.

Wakakutana na Azam katika mechi ya fainali ambapo mabao mawili ya Kiiza na Said Bahanuzi yaliwapa ushindi wa 2-0 dhidi ya Lambalamba na kuweza kutetea ubingwa.

Ikiwa imepita miaka takribani mitatu sasa, Azam leo wanaingia kucheza nusu fainali ya pili ya Kombe la Kagame  dhidi ya KCCA ya Uganda katika uwanja ule ule uliotumika mwaka 2012 dhidi ya AS Vita na kocha ni yule yule, Stewart Hall.

Mechi ya kwanza ya kundi C, Azam waliifunga KCCA 1-0 , goli la John Bocco ambaye pi alifunga goli katika nusu fainali ya mwaka 2012 dhidi ya AS Vita.


Je, histori ya nusu fainali ya 2012 inaweza kujirudia uwanja wa Taifa?...Tusubiri dakika 90 au 120....

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video