Mudathir Khamis
YANGA SC ipo katika harakati za kumsajili Golikipa wa KMKM
na Taifa Stars, Mudathir Khamis, ingawa timu hizo mbili zimelazimika kukaa tena
mezani kujadili ada ya uhamisho.
Stori ni kwamba, Yanga waliweka ofa yao mezani, KMKM wakaitosa,
lakini sasa wameamua kupunguza na kufungua taa ya kijani kwa Yanga.
Timu hizo zipo katika mazungumzo kwa mara nyingine na kwa
mujibu wa katibu wa Yanga, Dr. Jonas Tiboroha wanaweza kumalizana mapema Juma
lijalo.
Mtandao huu umemtafuta Dr. Tiboroha kutaka kujua maendeleo ya mazungumzo ya Yanga na KMKM.
Swali: Vipi kuhusu usajili wa Golikipa
kutoka KMKM, Mudathir Khamis?, inafahamika kwamba mlishindwana ada ya uhamisho,
lakini KMKM wameonekana kutaka kupunguza na mmelazimika kukaa tena mezani, hili
limekaaje?
Dr. Tiboroha: Hili naomba kwanza tusiongelee leo,
tutaongelea Jumatatu au Jumanne, (anacheka) bado liko jikoni, maendeleo ni
mazuri.
Swali: Mbona kama taarifa hii
imekushangaza?
Dr. Tiboroha: Hahahahaha! Kwa kweli
sikuelewi kabisa yaani!, unafanya kazi kubwa!, hongera sana! Lakini Mungu
akijaalia atavaa jezi ya Yanga msimu ujao (Mudathir).
Tutakuletea taarifa rasmi Jumatatu au Jumanne kama
alivyosema katibu mkuu wa Yanga…..
0 comments:
Post a Comment