Saturday, July 11, 2015

Na Ramadhani ngoda.
Matajiri wa jiji la Manchester klabu ya Manchester City imewawia kusubiri kabla ya kukamilisha usajili wa kiungo wa Aston Villa, Fabian Delph baada ya mkewe kukaribia kujifungua.
Delph ambaye amekamilisha asilimia kubwa ya uhamisho wake kuelekea Etihad kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 8 na kufikia makubaliano ya mkataba wenye thamani ya pauni 100,000 kwa wiki, anakwenda moja kwa moja kuziba pahala palipoachwa na Muingereza mwenzake James Milner aliyetimkia kwa majogo wa jiji Liverpool hivi karibuni.
Hii inamfanya Delph asijumuike mapema na City katika maandalizi ya msimu mpya hasa safari ya timu hiyo ya nchini Australia mpaka pale atakapokamilisha usajili wake uliobaki katika hatua ya vipimo vya afya tu.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Uingereza kutoka Villa Park ameahidiwa kupata nafasi kama aliyokuwa akiipata Milner katika kikosi hicho kinachonolewa na Mchile Manuel Louis Pellegrini.
Delph anatarajiwa kuwa sehemu ya mpango wa Manchester City wa kuongeza idadi ya wachezaji wazawa wakihitaji pia kwa udi na uvumba saini ya winga mwingine wa kingereza Raheem Sterling kutoka kwa majogoo wa jiji Liverpool kwani msimu uliomalizika ni Milner na aliyekuwa akicheza kwa mkopo, kiungo Frank Lampard ndio wachezaji wazawa pekee waliopata nafasi ya kuanza katika michezo Zaidi ya 10 katika michuano yote.
Katika hatua nyingine, ni kauli ya ‘kata mti panda mti’ kwa Aston Villa ambao wameziba pengo la Delph kwa kumnasa kiungo wa Lille Metropole ya Ufaransa, Iddrisa Gueye siku ya Ijumaa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video