Tuesday, July 7, 2015


Bondia asiyepigika, Floyd Mayweather amevuliwa mkanda wa ubingwa wa WBO, uzito wa Welterweight  unaohusisha kilo 67 na 77 ambao alishinda mwezi Mei mwaka huu dhidi ya Manny Pacquiao kutokana na  kushindwa kufuata sheria na kanuni za Shirikisho hilo.

Kamati ya mashindano ya WBO imesema kwamba haina jinsi ya kufanya zaidi ya kumvua mkanda huo Mayweather ambaye ameshindwa kulipa ada kutoka kwenye pambano alilopigana na Pacquiao.

Ijumaa iliyopita, ilikuwa siku ya mwisho kwa  Mayweather kutimiza vigezo vya ubingwa wa WBO ikiwemo kulipa ada ya dola laki mbili kutoka katika pambano lake na Pacquiao pamoja na kujivua ubingwa wa uzito wa light-middleweight wa WBC na WBA.

Mayweather (left) has been stripped of the WBO title he won in defeating Manny Pacquiao
Mayweather  anayetajwa kuwa mwanamichezo tajiri zaidi Duniani ameshindwa kutelekeza agizo hilo, hivyo kamati imeamua kumvua mkanda  wake wa kwanza wa WBO.

Bondia Timoth Bradley Jr anatarajiwa kupewa mkanda huo baada ya mwezi uliopita kumpiga kiutata,  Jessie Vargas  katika pambano la kutafuta bingwa wa muda wa uzito huo, ingawa Mayweather mwenye umri wa miaka 38 amepewa siku 14 za kukata rufaa.


Mayweather bado anashikilia ubingwa wa welterweight na super-welterweight  wa WBC na  WBA,  ingawa kisheria,  bondia haruhisiwi kushika ubingwa wa dunia kwa madaraja mbalimbali.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video