Friday, July 10, 2015


MAAFISA wa FC Lupopo ya DR Congo wametua makao makuu ya Yanga, mitaa ya Jangwani, Kariakoo, Dar es salaam kudai fedha za usajili wa Mbutu Twite.
Mwaka jana, Yanga walikubaliana na Lupopo kumsajili Twite kwa mkataba wa miaka miwili, lakini mabingwa hao wa Kandanda Tanzania bara wakaamua kumsainisha mwaka mmoja.
Baada ya mkataba huo kumalizika, Yanga wamemuongeza mwaka mwingine na  Lupopo waliposikia Twite kaongeza mwaka mwingine, wakajua Wanajangwani wameenda kinyume na makubaliano ya awali.
Wakafunga safari  kuja Dar es salaam na jana wamekutana na katibu mkuu wa Yanga, Dr. Jonas Tiboroha wakidai waongezwe hela za usajili wa Twite, lakini Daktari huyo wa michezo amewapa maelezo ambayo wameonekana kuridhika.
Dr. Tiboroha amezungumza na mtandao huu na kuthibitisha kwamba viongozi wa Lupopo wamefika Ofsini kwake.
“Hii ishu ilitatuliwa toka mwaka jana, kwanza nikupongeze!, umeipataje hii taarifa? Yanga mwaka jana walifikia makubaliano na FC Lupopo, ilifanya mazungumzo na Rais wa FC Lupopo, Bwana Kasongo na kukubaliana Yanga itoe kiasi ilichotoa (hajataja) ili iweze kumsajili Mbuyu Twite kwa miaka miwili”. Amesema Tiboroha na kuongeza: “Mwaka jana Mbuyu Twite alitakiwa asaini kwa miaka miwili, lakini Yanga baada ya kufanya makubaliano ilimsajili kwa mwaka mmoja”.

“Kilichowashangaza Lupopo mwaka huu ni kusikia Mbuyu Twite ameongeza mkataba wa mwaka mwingine,wam ekuja kudai hela. Walipofika jana, mimi nikaingia kwenye nyaraka na kuwaonesha vitu, kilichonishangaza pia ni kwamba wanadai yale makubaliano hawakuyapata japokuwa walipokea hela bila kupata mkataba wowote. Haya mambo tumeyaongea vizuri jana na wameonekana kuelewa”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video