Tuesday, July 14, 2015

Na Simon Chimbo;
Kwa wengi nchini Argentina, soka ni moja ya vitu wanaviabudu sana. Katika jimbo alilozaliwa mshambuliaji Carlos Tevez, Buenos, ndipo lilipo kanisa la gwiji wa soka duniani, Diego Armando Maradona.

Kanisa hili lilianzishwa na watu watatu Hernan Amez, Alejandro Veron na Hector Campomar mwaka 2001.

Kanisa hili limepata umaarufu mkubwa sana duniani kote huku likiwa na Tovuti yenye wafuasi katika nchi za Hispania, USA, Mexico, Afghanistan na Ufilipino.

Hili ni kanisa ambalo waumini wake humuabudu gwiji huyo Diego Armando Maradona na kwamba ndio Mungu wao.

Waumini wa kanisa hili, hufika kanisani hapo na kuanza kumuomba gwiji huyo kama Mungu wao huku kukiwa pia na sala zinazomtaja Diego Armando Maradona.

Katika ibada za kawaida, badala ya kutumia biblia, makasisi huwasomea kitabu ya historia ya mchezaji huyo, 'Autobiography'.

Wakati wa sherehe za misa kama ndoa, ubatizo na mambo mengine hufanyika siku ya kuzaliwa Diego Maradona yaani October 30. Hii ni siku kubwa sana kwa wafuasi wa dini hii duniani kote.

"Ni muhimu kumuonesha mapenzi, 'El Diego' kutokana na miujiza mingi tuliyoipata kupitia jina lake" anaeleza kasisi Amez mmoja wa waanzilishi wa kiroho wa kanisa hilo miaka kadhaa iliyopita.

Katika jengo hilo la kanisa, kuna alama za 'D10S' ambapo 10 ni utambulisho wa jezi namba aliyokuwa akivaa enzi zake uwanjani, lakini linatengeneza neno kama Dios ambalo humaanisha 'Mungu' kwa lugha ya kihispaniola.

Amez ambaye ni Padre wa kanisa hilo anamzungumzia Lionel Messi kama mmoja wa wanasoka adimu duniani na kummwagia sifa kibao huku akitoa siri kwamba Messi alikua ni moja kati ya watu wa kwanza kufika kanisani hapo kuchukua jezi iliyosainiwa na 'Mungu' Maradona na kisha kuipeleka Barcelona.

"Watu wote hupita mitaani kote tukikumbatiana na kushangilia. Tunasahau tofauti zetu zote za kisiasa na kijamii kumtukuza El Diego. Hakuna mtu mwenye uwezo wa kutuunganisha kama Maradona"- anaeleza padri huyo Amez wa kanisa hilo.

Tarehe nyingine muhimu ni 22 June ambapo huifanya kama ndio Pasaka katika kanisa hilo. Siku hiyo ni siku ambayo mfalme huyo wa soka duniani, alifunga goli la mkono dhidi ya England katika fainali za kombe la dunia mwaka 1986.

Bwana Amez anasema goli na siku hiyo haitosahaulika sio tu duniani bali na mbinguni.

Lakini baada ya kukosolewa vikali na baadhi ya watu na dini mbalimbali ulimwenguni kote kuhusiana na kanisa hilo, padri Amez anakuja na utetezi huu, "sisi hatuingiliani na dini zingine za ukristo. Tunamuabudu Maradona katika soka tu na sio vinginevyo. Wengi wetu hapa ni waumini wa kanisa katoliki lakini kuhusu soka, El Diego ndio 'mungu' wetu".

Inaelezwa kuwa mshambuliaji wa zamani wa Barcelona na England, Gary Linekar ambaye ni mchambuzi maarufu wa soka hivi sasa pamoja na kocha wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettinho ni waumini na wanakadi za uumini wa kanisa hilo.

KIPI KINAVUTIA HAPA?

Wakati waumini wakiabudu kanisani, El Diego mwenyewe huwa akifanya shughuli zake ikiwa hata kunywa bia na mambo mengine kwa kuwa yeye sio mchungaji wa kanisa hili bali yeye ni 'mungu' hivyo waumini wanawajibu wa kwenda kuabudu kanisani hapo na kukutana na wachungaji ambao ndio viongozi wa kanisa.


Lakini pia kama ukitaka kubatizwa kanisani hapo ni lazima ukubali kuitwa 'Diego' kama jina lako la katikati ili kumpokea kikwelikweli gwiji huyo kuwa ndio 'mungu' wako wa soka.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video