Monday, July 6, 2015


Na Ramadhani ngoda.

Licha ya kukanusha taarifa za Paul Pogba kuwa njiani kuelekea Fc Barcelona kutokana na mzungumzo ya wiki iliopita, raisi wa Juventus Turin, Andrea Agnelli amekiri kuwa kiungo huyo muda wowte ataondoka klabuni hapo katika majira haya ya joto.

Matajiri wa jiji la Manchester klabu ya Manchesetr City wanaaminika kuwa wako tayari kutoa kiasi kinachohitajika na vibibi vizee hivyo vya jiji la Turin cha pauni milioni 70, lakini kiungo huyo anaweza kuwa na nafasi kubwa Zaidi ya kujiunga na mabingwa wa Hispania na Ulaya, Fc Barcelona.

Mabingwa wa Ufaransa PSG wakiwa miongoni mwa timu zinazowania dole gumba la kiungo huyo, moja ya watu wanaowania nafasi ya uraisi katika klabu ya Fc Barcelona Juan Laporta, amemuweka Pogba kama sehemu ya ahadi katika kampeni zake mwaka huu.

Kauli ya kuonesha kukata tamaa kwa Juve juu ya Pogba iliyotokewa na raisi Agnelli imekuja ikiwa ni wiki moja tu tangu akanushe vikali fununu za Mfaransa huyo kuelekea Camp Nou ambapo Barca walikuwa tayari kumuacha kwa msimu mmoja Juventus kutokana na adhabu yao ya kutosajili.

“Hakuna kilichopo kwa 100% katika soka. Unaweza kusema mchezaji hauzwi kuanzia tarehe 1 Septemba (dirisha litakuwa limefungwa),” alisema Agnelli katika mkutano na waandishi wa habari.

“Miaka kadhaa iliyopita, tulisema Christian Vieri hauzwi, lakini alielekea Atletico Madrid siku chache tu zilizofuata,” alisisitiza raisi huyo.

Pogba (22) aliyebakisha miaka mine kwenye kanfarasi yake Juventus, ameshaiwakilisha timu yake ya taifa katika ngazi zote na ameshashinda ligi kuu Italia mara 3, na kuisadia timu yake kufika fainali na ligi ya mabingwa msimu uliyomalizika na kushuhudia Barcelona wakiibuka machampioni.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video