Wednesday, July 8, 2015


Na Ramadhani Ngoda.
Licha ya uvumi uliotanda kuwa anaweza kuondoka Santiago Bernabeu, mlinzi wa klabu hiyo Mhispania Dani Carvajal amejitia kitanzi kwa kuongeza mkataba wake utakaomuweka Bernabeu hadi 2020.

Awali tetesi zilieleza kuwa mlinzi huyo wa kulia angeweza kumpisha Mbrazil Danilo Luiz Da Silva aliyesajiliwa akitokea Fc Porto ya nchini Ureno na kuonekana kuwa katika malengo ya kocha mpya Rafa Benitez.

Mlinzi huyo wa kimataifa wa Hispania ambaye alibakisha miaka 4 kwenye mkataba wake, ameamua kupigana kupata namba ndani ya mabingwa hao wa Ulaya wa mwaka 2014 licha ya kuwa na upinzani kutoka kwa Danilo.

Carvajal (23) alitokea kwenye timu ya vijana ya Real kabla ya kutimkia nchini Ujerumani kunako klabu ya Bayer04 Leverkusen mwaka 2012.

Madrid walifanikiwa kumrudisha beki huyo msimu uliofuata kutokana na mkataba wake kuwa na kipengele ambacho kingeweza kumrejesha Bernabeu wakilazimika kulipa kiasi cha Yuro milioni 6.5 tu na baada ya kukaa Bayarena kwa msimu mmoja pekee.

Tangu kurejea kwake amekuwa akipata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza cha miamba hiyo ya mji mkuu wa Hispania na kuwa sehemu ya kikosi kilichoshinda ligi ya mabingwa na Copa Del Rey msimu wa 2013/14 chini ya kocha ‘aliyetalikiwa’ Carlo Anceloti.




0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video