Friday, July 31, 2015


Viungo washambuliaji wa klabu ya arsenal ya jijini London, Theo Walcott na Santiago Cazorla wamesaini mikataba mipya itakayowakikishia kubaki pale Emirates.

Theo Walcott ambaye amefunga magoli 76 katika mechi 302 akiwa na washika bunduki alijiunga na klabu hiyo akitokea pale Saint marry mwaka 2006. Amesaini mkataba wa miaka 4 na atakuwa analipwa kitita cha Euro 140, 000 kwa wiki na kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa mishahara ya juu pale Emirates.

 Mchezaj huyo mwenye miaka 26 alimaliza msimu kwa staili nzuri baada ya kupiga “hatrick” kwenye mechi ya mwisho dhidi ya West Brom, pia alifunga kwenye ushindi mnono wa magoli 4 dhidi ya Aston Villa kwenye fainali ya FA.

Pia kiungo matata kutoka Hispania, Santiago Cazorla mwenye miaka 30 pia amesaini mkataba wa miaka 2. Cazorla amecheza mechi 148 tangu ajiunge na Arsenal kutoka Malaga huku akifunga magoli 27 likiwemo goli
la fainali ya FA mwaka 2014.

Inawezekana mikataba hii ikazidi kuwanufaisha arsenal, kwani wachezaji hawa ni muhimu sana katika kikosi cha Wenger ambacho kinatarajiwa kutwaa ubingwa msimu ujao wa EPL.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video