Na Ramadhani Ngoda.
Nahodha wa zamani wa
klabu ya Liverpool, Steven Gerrard ameamua ‘kumchana makavu’ nyota wa klabu hiyo
anayeuumiza kichwa uongozi wa Liverpool Raheem Sterling na kumwambia awe ‘mwanaume’
na kuwa na msimamo juu ya mstakabali wake Anfield.
Sterling ambaye kwa
sasa amerejea mazoezini baada ya kukosekana kwa siku mbili ikidaiwa kushinikiza
klabu hiyo kumuuza ilihali majogoo hao wa jiji bado wanahitaji huduma ya mzawa
huyo wa Jamaica.
Ktika mahojiano
maalumu na sky sports makao makuu, Gerrard amesikitishwa na tabia chafu ya winga
huyo na kukiona kitendo hicho kuwa si cha kiungwana kwa wapenzi wa klabu hiyo
walioonesha kumthamini na kumpenda kipindi chote cha maisha yake Liverpool.
“Raheem anatakiwa
aingie ndani na aongee na wamiliki wa klabu na Brendan (Rodgers) mwenyewe,
awaeleze nini anataka,” alisema Gerrard.
“Kuna mamilioni na
mamilioni ya mashabiki wa Liverpool duniani
kote wanaopenda kumuona Raheem akiwa kwenye jezi ya Liverpool. Hivyo
sidhani kama ni vizuri kwao kusikia anafanya vitu kama hivi,” aliongeza nahodha
huyo wa zamani wa Liverpool.
Kuonesha bado
Liverpool inamuhitaji Sterling, tayari miamba hiyo ya England imeshakataa ofay
a Manchester City ya pauni milioni 40 kutoka kwa matajiri wa jiji la
Manchester, Manchester City.
Licha ya Sterling
mwenyewe kukiri kuwa yeye hasukumwi na pesa katika maamuzi yake, bado wakala
wake Aidy Ward alishasema kuwa Raheem asingesaini mkataba mpya na Liverpool hata
kama ungemlipa pauni 900,000 kwa wiki.
0 comments:
Post a Comment