Tuesday, July 7, 2015


Na Ramadhani ngoda.
Kiungo wa kimataifa wa Algeria na klabu ya Tottenham Hotspur, Nabil Bentaleb hatimaye amefikia makubaliano ya kusaini mkataba wa miaka 5 utakaomuweka White hart Lane hadi mwaka 2020.

Mazungumzo juu ya mkataba mpya na kiungo huyo almanusra yagonge mwamba msimu uliopita huku Mualgeria huyo akionesha kuchoshwa na kucheleweshwa kwa hatma yake klabuni hapo lakini sasa mambo yamekwenda sawa bin sawia na nyota huyo ataendelea kuonekana akiwa na uzi wa Spurs.

“Klabu inayo furaha kutangaza kuwa Nabil Bentaleb amesaini mkataba mpya wa miaka 5 utakadumu hadi 2020,” ulisomeka ujumbe ulioandikwa kwenye ukurasa maalum wa twita wa klabu hiyo yenye maskani yake Kaskazini mwa London.

Bentaleb (20) amefurahishwa na hatua hiyo na kuashidi kujituma kwa nguvu zake zote awapo uwanjani ili kufikia malengo ya klabu kwani ndio kinachohitajika kwa mchezaji aliyethaminuiwa na klabu kwa kupewa mkataba mpya jambo linaloonesha bado anaaminika na kuthaminiwa.

“Kwa kweli nina furaha sana kujifunga na klabu hii hadi 2020,” Bentaleb aliiambia tovuti ya klabu hiyo.

“Klabu imeniamini ni lazima niwashukuru kwa hilo na kuzidi kuongeza jitihada ili kufikia lengo,” alisisitiza Bentaleb.


Bentaleb ambaye alikuwa mchezaji muhimu kwa Spurs msimu wa 2013/14 chini ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Tim Sherwood, bado anaonekana kuwa miongoni mwa wachezaji muhimu katika kikosi cha kocha Mauricio Pochetino.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video