Monday, July 6, 2015


Na Ramadhani Ngoda.
Mabingwa wa Hispania na Ulaya, Fc Barcelona hatimaye wameshinda mbio za kuwania saini ya kiungo wa kimataifa wa Uturuki na klabu ya Atletico Madrid, Arda Turan baada ya kuthibitisha kumtia mikononi nyota huyo kwa ada ya uhamisho ya Yuro milioni 34 huku ikitarajiwa kupanda hadi kufikia milioni 41 kutokana na vipengele vya mkataba wake.

Barcelona wanaweza kumuacha Turan Atletico kama raisi wao ajae ataamua hilo kutokana na kutumikia adhabu yao ya kutosajili miaka miwili.

Kuemekuwa na tetesi nyingi juu ya hatma ya Mturuki huyo hasa baada ya kutangaza wazi kuwa asingeongeza mkataba na Atletico Madrid na vilabu mbalimbali kuibuka kutaka huduma yake miongoni mwao wakiwepo mabingwa wa Uingereza Chelsea.

Mapema wiki iliyopita muwania nafasi ya uraisi wa miamba hiyo ya Catalan, Josep Maria Bartomeu aliweka wazi nia yake ya kutaka kumnasa winga huyo akidai kuwa kocha wa mabingwa hao Luis Enrique Martinez anamuhitaji kwa udi na uvumba mchezaji huyo.

“Rasmi, Barcelona inatangaza kumsajili Arda Turan. Karibu Arda,” ulisomeka ujumbe katika ukurasa wa twita wa klabu hiyo.


Wanaowania uraisi katika klabu ya Barcelona wamekuwa na ahadi kede kede za kusaini nyota mbalimbali endapo tu watachaguliwa kuiongoza Barcelona katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Julai 8 mwaka huu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video