Na Ramadhani ngoda.
Baada ya Mturuki Arda
Turan kukamilisha usajili wake kuelekea Fc Barcelona, Atletico Madrid haraka
wamemsajili winga wa Kibelgiji anayekipiga kunako klabu ya AS Monaco, Yannick
Ferreira Carrasco kama mbadala wake.
Winga huyo wa
kimataifa wa Ubelgiji amesaini mkataba wa miaka 5 na miamba hiyo ya jiji la
Madrid baada ya makubaliano ya kukamilisha dili hilo kwa ada ya uhamisho wa
pauni milioni 14.3 kufikiwa na pande zote mbili.
Carrasco ambaye mpaka
sasa amekwishaichezea timu ya taifa ya Ubelgiji michezo 9, anaoneka kuwa mrithi
sahihi wa viatu vilivyoachwa na Arda Turan aliyetimkia Camp Nou hivi karibuni.
“Tumeridhishwa sana
na makubaliano yaliyofikiwa kati yetu na Monaco. Kwa sababu Yannick (Carrasco)
ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa na muelekeo mzuri,” alisema mkurugenzi wa
michezo wa Atletico Madrid, Jose Luis Perez Caminero baada ya
kukamilika usajili huo.
“Anacheza kwa kasi kubwa sana, ni mzuri
katika kukokota mpira na ana uwezo mzuri wa kupiga mashuti. Atakuwa na mchango
mkubwa sana katika lengo letu na kuongeza ubora wa timu yetu na ushindani pia,”
aliongeza Caminero.
Carrasco sasa anakuwa ingizo jipya la
tatu Vincente Calderon baada ya kusajiliwa kwa nyota wawili, Jackson Martinez
na Luciano Vietto huku mwalimu Diego someone bado akiangalia uwezekano wa
kuongeza nyota wengine ili kuboresha kikosi chake kilichokosa ubingwa msimu
uliomalizika.
0 comments:
Post a Comment