Monday, July 6, 2015


Na Ramadhani Ngoda.
Mchezaji wa tenisi namba 3 kwa ubora duniani Muingereza Andy Murray amewatoa kimaso maso Waingereza baada ya kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Wimbledon inayoendelea katika ardhi ya nyumbani kwao kwa kumchapa Mcroatia Ivo Karlovic kwa seti 7-6 (9-7) 6-4 5-7 6-4.

Murray (28) licha ya kulinda heshima katika ardhi ya nyumbani, hii kwake ni mara ya 18 mfululizo kutinga robo fainali katika michuano mikubwa ya mchezo huo na sasa atapumzika siku moja kabla ya kumvaa Mcanada, Vasek Pospisil siku ya Jumatano (Julai 8).

Licha kushinda mchezo huo, Murray alikiri kupata changamoto kubwa kutoka kwa Mcroatia huyo na kamwe jaikuwa kazi rahisi kwake kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

“Kiukweli ilikuwa mechi ngumu sana. Kiakili ilikuwa inachosha kwa sababu inabidi uwe tayari kwa kila nafasi inayotokea,” alinena Murray baada ya mchezo.

Kikwazo cha Mrray kutinga nusu fainali ya michuano hiyo kinabaki kuwa ni Vasek Pospisil aliyemuondosha Muingereza James Ward katika mzunguko wa tatu na baadaye kumgaragaza Viktor Troicki.

Mzawa huyo wa Glasgow inambidi kufanya kazi ya ziada kama kweli anahitaji taji hilo lisitoke nje ya ardhi ya nyumbani yanakofanyikia mashindano hayo.





0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video