Wednesday, June 10, 2015


Singano akiwa ametulia nyumbani kwao Keko, Machungwa, Dar es salaam

SHIRIKISHO la soka TanzaniaTFF limezitaka klabu kushirikiana na SPUTANZA pamoja na Bodi ya Ligi katika kuweka mifumo mizuri ya uingiaji mikataba. 

 TFF inao mkataba mama (template) ambao klabu zote na wachezaji wanatakiwa waufuate wakati wanaandaa mikataba yao (individual contracts between players and clubs).  

Hayo yamekuja baada ya kuibuka kwa utata wa mkataba wa Ramadhan Singano ‘Messi’ na klabu yake ya Simba.
Singano alikuwa na mkataba wa miaka miwili unaoisha mwezi Julai mwaka huu 2015, wakati Simba wao walikuwa na mkataba wa miaka mitatu utakaoisha mwezi Julai mwakani.
Katika kikao cha jana ambapo TFF iliwakutanisha Singano na Simba, pande zote zilieleza kutambua utata ulio ndani ya mikataba iliyokuwepo ambayo kimsingi iliingiwa kabla ya uongozi wa sasa wa Simba SC.

Kwa pamoja pande hizo mbili zimekubaliana kuanza mazungumzo ya makubaliano mapya na hatimaye mkataba mpya utakaoanza katika msimu mpya wa 2015/16.
Kutokana na maamuzi hayo, Singano ametoa kauli hii: “Wamesema tukae chini tuongee, mikataba yote haipo, kisheria mimi niko huru” “Tukishindwa kukubaliana inabidi nitafute timu nyingine, lakini kipau mbele ni kuongea nao (Simba) kama kweli wana nia au hawana nia na mimi”.
Hata hivyo Singano alitamka bayana kuwa hawezi kuelewana tena na Simba na hii inaashiria safari ya kutua Azam fc inanukia.
Azam fc wana mpango wa kumsajili Singano endapo utata wa mkataba wake utamalizika na walishaeleza wazi kuiwania saini yake.

Kikubwa inabidi nipewa mkataba niangalie na kuweka vitu vyangu. Niwashauri wachezaji wenzangu, bora ukose vitu vyote kuliko kukosa mtu wa kukuongoza, ukikwama utasaidiwa

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video