Monday, June 1, 2015


KOCHA msaidizi wa Kagera Sugar Mrage Kabange naye amepewa mkono wa kwa heri toka kwa wakata miwa wa mkoni Kagera baada ya mkataba wake na ‘wana Nkurunkumbi’ kumalizika mwishoni mwa msimu huu.

Kabange ambaye ni mchezaji wa zamani wa klabu ya Simba SC, ameitumikia Kagera Sugar kwa muda wa miaka nane lakini baada ya mkataba wake kumalizika msimu huu hakupewa mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo inayomilikiwa na kiwanda cha kutengeneza sukari cha Kagera Sugar kilichopo mkoani Kagera.

Winga huyo wa zamani wa Wekundu wa Msimbazi amesema, milango ipo wazikwa klabu yoyote inayohitaji huduma yake yeye yupo tayari kufanya nao mazungumzo na kama watafikia makubaliano basi watafanya kazi pamoja.

“Sina sehemu yoyote ninayopenda kuelekea, ila milango yangu ipo wazi kwa mtu yeyote yule ambaye anaona naweza kumsaidia basi aniite tuzungumze halafu tutajua nini kitaendelea lakini mimi sina mahali popote kusema napendelea kwenda hapa au pale. Timu yoyote tukayofikia nayo makubaliano mimi nikotayari kufanya nayo kazi”, amesema Kambange.

“Nawashuhuru sana Kagera Sugar nimeishi nao kwa wema wale jamaa, hakuna ubaya hata mmoja wala chuki, sijawahi kugombana na viongozi, wanachama wala wapenzi wa Kagera Sugar. Nimeishi kwa amani na nimeondoka kwa amani, lakini wao walichosema baada ya mkataba kumalizika ni kwmba, wanahitaji sura mpya ambayo pengine wanaona inaweza kuwafikisha mahali pengine kutoka pale ambapo tumeiacha sisi”, Kabange aliongeza.

“Kwa mujibu wa katibu wa timu, malengo ya Kagera Sugar yalikuwa ni kumaliza ligi timu ikiwa kwenye nafasi tatu za juu yaani nafasi ya tatu, ya pili na kuendelea, sasa sisi hatukuweza kufika katika nafasi hizo”, alimaliza Kambange.


Baada ya kocha huyo kumalizana na timu yake ya Kagera Sugar, kumekuwepo na taarifa kwamba Simba SC wanamnyatia kocha huyo ili atue kwenye benchi la ufundi la Wekundu wa Msimbazi kwa ajili ya kuliongezea nguvu benchi hilo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video