Thursday, June 18, 2015

Klabu ya Yanga imethibitisha kuvunja mkataba na mshambuliaji wake, Said Bahanuzi kutokana na kushuka kiwango kwa miaka mitatu mfululizo.
Katibu mkuu wa Yanga, Dkt. Jonas Tiboroha amesema kwamba , Yanga haijaridhishwa na maendeleo ya Bahanuzi aliyekuwa anacheza kwa mkopo msimu uliopita katika klabu ya Polisi Morogoro, hivyo anatolewa kama ilivyotokea kwa Jeryson Tegete na Omega Seme.


“Bahanuzi ni moja ya wachezaji tuliovunja nao mikataba kwasababu klabu haijaridhishwa  na maendeleo yake  kama ilivyo kwa wachezaji wenzake  akina Omega, Thabit, Jerry Tegete”. Amesema Tiboroha na kuongeza: “Mikataba ya Yanga inaangalia  kiwango cha mchezaji, kama mchezaji hana kiwango kwa miaka mitatu anaachwa, tunavyo vipengele vinavyoeleza wazi”. Amesema Toboroha.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video