Monday, June 1, 2015

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam
KIUNGO-mshambulizi, Deus Kaseke, mlinzi wa kushoto, Hajji Mwinyi, golikipa, Benedictor Tinocco na mshambulizi, Malimu Busungu tayari wamesainiwa na Yanga SC kuelekea msimu wa 53 wa ligi kuu na michuanno ya klabu bingwa Afrika mapema mwaka ujao.

 Nyota hao wanne kutoka klabu ya Mbeya City FC, KMKM ya Zanzibar, Kagera Sugar na JKT Mgambo ni mapendekezo ya mwalimu wa timu hiyo, Hans Van der Pluijm na kwa mara ya kwanza tunaweza kuona Yanga wakifanya usajili ambao naweza kuuita ' Usajili wa Kitaalamu'.

Tinocco ambaye aliidakia Kagera msimu uliomalizika Mei mwaka huu ni kipa wa timu ya pili ya Taifa ' Taifa Stars Maboresho' atachukua nafasi ya mlinda mlango mzoefu, Juma Kaseja ambaye alijitoa katika timu hiyo miezi 6 iliyopita kwa sababu ya kushindwa kuwa kipa chaguo la kwanza mbele ya Deogratius Munishi ' Dida' na Ally Mustapha ' Barthez'.

Kwa muda mrefu wapenzi wa timu hiyo wamekuwa na mashaka na upande wao wa ulinzi ' beki namba 3'. Kimsingi kwa misimu minne sasa tangu kuondoka kwa Amir Maftah katikati ya mwaka 2011, nafasi ya mlinzi wa kushoto ' ime-hodhiwa' na Oscar Joshua.

Wakati fulani walitokea Stefano Mwasyika na David Luhende. Wawili hao ( Mwasyika na Luhende) walikuwa na mtazamo wa kushambulia zaidi kuliko kuzuia katika uchezaji wao ndiyo maana walimu, Kostadin Papic, Sam Timbe, Tom Saintfiet, Ernie Brandts na Hans walipendelea kuwatoa pia katika winga ya kushoto.

Oscar ameifanya Yanga kuwa ngumu kupitika katika upande wa kushoto, licha ya kutopendelea kupanda na timu kwenda mbele, Oscar hutumia nguvu zake kushambulia kwa mipira mirefu inayofika kwa walengwa.

Lakini Yanga haikupaswa kuendelea kumuacha mcheza wa pekee katika nafasi hiyo ndiyo maana mwalimu Hans wakati fulani alinukuliwa akisema kuwa angependa kuona timu yake ikimsaini kwa mara nyingine, Luhende ambaye aliachwa katika usajili wa mwaka uliopita baada ya Mholanzi huyo, Hans kupata kazi Uarabuni.

Mwinyi ni nyongeza katika beki 3 ya Yanga na mchezaji ambaye ataleta changamoto na tofauti kwa Oscar.

Ni mlinzi wa timu ya Taifa ya Zanzibar na ile ya Tanzania. Wengi tunauchukulia usajili wa Kaseke kama ' mbadala' wa kiungo mshambulizi, Mrisho Ngassa ambaye amejiunga na klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini, lakini ikumbukwe kuwa Yanga itawapoteza wachezaji kama Nizar Khalfan ambaye amejiunga na Mwadui FC ya Kahama, Shinyanga, Hassan Dilunga ameshindwa kumshawishi, Hans licha ya kupewa nafasi ya kucheza mara kwa mara hivyo naye ataondolewa.

Kaseke ni kiungo ambaye ana uwezo wa kucheza upande wa kushoto, kulia na hata kiungo wa mashambulizi ' namba 10'.

Yanga ilimuhitaji mchezaji kama Kaseke ambaye atakuwa na uwezo wa ' kuinyanyua' timu hata ikiwa ' dhohofu' na kuifungia magoli magoli. Akiwa na miaka 21 sasa, mchezaji huyo amejijenga kimchezo katika misimu miwili katika kikosi cha City.

Tayari amecheza jumla ya michezo 51 ya ligi kuu Bara na kufunga jumla ya mabao 8. Ataweza kufanya kazi ya Ngassa?. Kukimbia kwa kasi katika nafasi, kucheza kwa kuhaha eneo lote la mashambulizi akijaribu kufunga na kutengeneza nafasi za magoli. Tusubiri na tuone ila hadi amesajiliwa Yanga tunapaswa kuipongeza timu hiyo kwa usajili mbadala.

Yanga inahitaji wachezaji wawili au watatu zaidi wa nafasi ya kiungo. Haruna Niyonzima ni mchezesha timu mzuri, Salum Telela na Said Juma Makapu ni ‘ injini’ katikati ya uwanja. Hivyo hakuna wasiwasi sana na kuondoka kwa viungo kama Nizar na Dilunga.

Katika michuano ambayo inahitaji mbinu tofauti tofauti ili kupata matokeo, Yanga watalazimika pia kuutengeneza mfumo wa 4-4-2 ili uwasaidie katika Ligi ya Mabingwa na ligi kuu ijayo. Licha ya kumsaini mshambulizi, Busungu ambaye alifunga mabao kumi akiwa na Mgambo msimu uliomalizika, Yanga ina washambuaji kama Amis Tambwe, Kpah Sherman, na wakati mwingine huchezeshwa Saimon Msuva. Ndio walifunga magoli mengi katika msimu uliopita kutokana na mfumo ‘ ulio wakubali’ wa 4-3-3, lakini timu hiyo ilishindwa katika michezo mingi dhidi ya timu kubwa kwa kuwa walibanwa katika njia na hawakuwa na mbinu mbadala.

Katika gemu mbili na Simba SC walishindwa kufunga na walifunga goli moja tu katika michezo mitatu ya ugenini katika michuano ya komnbe la Shirikisho Afrika. Kwa nini imekuwa hivyo?.

Jibu ni kwamba wachezaji wa safu ya mashambulizi katika timu hiyo hawawezi kucheza katika mtindo wa ‘ washambuaji wawili’ kwa sababu wote hawana ujuzi wa kucheza kama mshambulizi wa pili-Namba 10.

Bahati mbaya kwa Tanzania hakuna mchezaji ‘ spesho’ ambaye anaweza kubeba majukumu hayo kwa sasa hivyo watalazimika kusaka ‘ namba kumi bora’ nje ya nchi ilitayewabeba katika michezo mikubwa.

Jerson Tegete amesaini Mwadui FC, Hussein Javu na Said Bahanzi muda wao umemalizika hivyo hawatakuwepo msimu ujao. Usajili wa Busungu umeletwa kuchukua moja ya nafasi hizo ila hautoshi.


0714 08 43 08

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video